Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) ametoa muda wa mwezi mmoja kwa mkandarasi wa mradi wa maji Tunduma kukamilisha kazi hiyo. 

Mhe. Aweso (Mb) ametoa muda huo mjini Tunduma baada ya kukagua mradi huo ambao umekamilika kwa asilimia 93 na kusisitiza atarudi kuufungua baada ya muda aliotoa kukamilika. Amesema wananchi wanasubiri majisafi na salama kutoka katika mradi huo ambao Serikali imetoa kiasi cha Shilingi milioni 895 kuhakikisha huduma inawafikia wananchi. 

Wakati huohuo, Mhe. Aweso (Mb) amewaelekeza Wahandisi wa Maji mkoani Mbeya kufanya kazi kwa weledi na kuepuka vishawishi ambavyo vinaharibu taaluma yao na kazi. Mhe. Aweso amesema hayo katika kikao kazi kilichowakutanisha Wahandisi wa maji wa mkoa wa Mbeya, jijini Mbeya. Amewaelekeza moja ya kazi wanayotakiwa kufanya ni kutembelea miradi na kujiridhisha na ubora wake, pia kujua kinachofanyika katika ujenzi na sio kukaa maofisini. 

Mhe. Aweso (Mb) amesema mradi ukijengwa katika kiwango bora na wananchi wakapata huduma nzuri jambo hilo ni moja kati ya kumbukumbu muhimu kwa wote waliofanya kazi, na kusisitiza wahandisi wote wanaofanya vizuri watatambuliwa kwa ubora wa kazi walizosimamia. 

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 
Wizara ya Maji na Umwagiliaji 
25.09.2018
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Jumaa Aweso (Mb), akiongea na Wahandisi wa Maji wa mkoa wa Mbeya kuhusu uwajibikaji katika miradi ya maji.
Wahusika walioshiriki katika kusimamia mradi wa Maji Galijembe mkoani Mbeya, Wahandisi wa majina na mkandarasi-kampuni ya Black Dot, wakiwa katika gari la Polisi ili kusaidia kuhusu mkandarasi kulipwa na mradi kutokamilika.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Jumaa Aweso (Mb), akiangalia maendeleo ya ujenzi wa chujio la maji katika mradi wa maji wa Vwawa mkoani Mbeya. 
Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo (kushoto) akimkaribisha Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) kuongea na watumishi wa Mamlaka ya Maji jijini Mbeya.
Watumishi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira jijini Mbeya wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Jumaa Aweso (Mb), hayupo pichani, jijini Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...