Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MSIMU wa pili wa Tuzo za Sinema Zetu Nchini zijulikanazo kama Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF) zimezinduliwa rasmi leo Jijini Dar es salaam na kumtangaza kwa  Mlezi wa tuzo hizo.
Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo alitangazwa kuwa mlezi wa tuzo za SZIFF kwa msimu wa pili na kuahidi kuhamasisha vijana kujikita zaidi katika ubunifu wa sanaa ya uigizaji.

Akizindua maandalizi ya tuzo hizo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Tido Mhando amesema kuwa anajivunia namna msimu wa kwanza wa tamasha la SZIFF lilivyoamsha ari na hamasa kwa waandaaji na wapenzi wa filamu nchini na fainali yake kufanyika 23 februari 2019.

Tido amesema, Hili ni tamasha la kwanza la Filamu Afrika kuonyeshwa kwenye televisheni , filamu zitashindanishwa kwenye vipengele tofauti huku ushindani ukiaminika kuwa mkubwa zaidi wa msimu uliopita kwakuwa moja ya vigezo vya filamu zitakazoshindanishwa ni kuwa lazima ziwe zimeandaliwa kati ya mwaka 2016 hadi 2018.

Amesema kuwa, mbali na hilo kwa mwaka huu wameongeza vipenele vingine vitano na kufikisha idadi ya  tuzo zinazowaniwa kuwa 24, pamoja na mshindi kuondoka na tuzo hiyo pia atakabidhiwa kiasi cha fedha taslimu kulngana na nafasi alizowania na kushinda.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe na Mlezi wa Tuzo za SZIFF Jokate Mwegelo amesema kuwa anafurahi sana kupewa nafasi ya kuwa mlezi wa tuzo hizo kwani hata yeye alikuwa  katika tasnia ya filamu akiwa amecheza filamu mbalimbali.

Amesema kuwa, tuzo hizi zimeleta chachu ya wasanii kufanya kazi kwa ubunifu mkubwa na kuhamasisha zaidi vijana kufanya kazi za sanaa kwani  inawapatia kipato wasanii wengi sana ila wanahitaji mtu wa kuwasaidia kuinua na tuzo hizi za SZIFF zimekuwa na mchango mkubwa sana.

Mkurugenzi wa Tamasha la SZIFF, Jacob Joseph amesema kuwa kiswahili ni miongoni mwa ligha kumi kubwa kuzungumzwa Barani Afrikla, matamasha mengi hayajakidhi kuwafikia watu wengi na kuwatimizia mahitaji yao kupitia sanaa.

fisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Tido Mhando(wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa msimu wa pili wa Tuzo za Sinema Zetu Nchini zijulikanazo kama Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF)  na kumtangaza  Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo  kuwa mlezi.
  Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo  akizungumza na wasanii waliojitokeza katika uzinduzi wa  msimu wa pili pili wa Tuzo za Sinema Zetu Nchini zijulikanazo kama Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF) na kwuashukuru waandaaji wa tamasha hilo lwa kumpa nafasi ya kwua mlezi wao.
 Mratibu wa tamasha la Sinema Zetu Nchini (SZIFF), Sophia Mgaza  
 akivitaja vigezo na tuzo zitakazowaniawa katika msimu wa pili wa Tuzo za Sinema Zetu.
Picha ya Pamoja ya waandaji wa Tuzo za Sinema Zetu, wasanii na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...