Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Mbeya

Mkurugenzi wa Shule za Patrick Mission na mdau wa Maendeleo Ndele Mwaselela ametoa msaada kwa wajane wawili katika kanisa la KKKT Forest Mkoani Mbeya .

Mwaselela ambaye alipata nafasi ya kuzungumza na wanakwaya wa kwaya ya Safina ya kanisa hilo, ambapo aliomba apewe wajane wawili Ili aweze kuwapa mitaji ya kujikwamua kimaisha.

“Mimi ni Mtoto wa Mama ntilie ambaye nimefanikiwa leo hivyo niwaambie wazi, Mama yangu alikuwa anauza Supu ili mimi nisome, hivyo nina kila sababu  ya kuwasaidia watu mbalimbali wasiojiweza wakiwemp wajane,binafsi naona fahari kila ninapofika mahali  angalau niweze kuwagusa wanawake wawili” alisema Mwaselela.

Mwaselela amesema kuwa mbali ya kuwa mtoto wa Mama Ntilie, walitokea watu wakainuka wakanisomesha na wengine sasa ni wabunge na wamepata kushika nafasi za juu serikalini.

Amesema kuwa ni vyema watu wakajifunza kutoa na kusaidia wengine, kwani kwa kufanya hivyo Mungu hugusa pale walipotoa na kuwabariki kwa kila hatua wanayopita.

Mwaselela alimaliza kwa kusema ni vyema jamii ya Watanzania  ijifunze namna ya kusaidia wengine kwa kile kidogo wanachokipata katika shughuli zao za kila siku.
 Mkurugenzi wa Shule za Patrick Mission na Mdau wa Maendeleo Ndele Mwaselela akizungumza wakati wa Ibada katika kanisa la KKKT Forest Mbeya juu ya umuhimu wa utoaji kwa jamii.
 Mkurugenzi wa Shule za Patrick Mission na Mdau wa Maendeleo Ndele Mwaselela, akikabidhi fedha kwa wajane ambao aliomba wasaidie katikati ya ibada
Mkurugenzi wa Shule za Patrick Mission na Mdau wa Maendeleo Ndele Mwaselela  akiombewa na Mchungaji  Kiongozi wa Usharika wa KKKT Forest Mbeya.

Mkurugenzi wa Shule za Patrick Mission na Mdau wa Maendeleo Ndele Mwaselela  akiagana na Mchungaji wa Usharika

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...