Zaidi ya asilimia 50 ya wakazi 8,000 wa Kata ya Ayamohe Wilayani Mbulu Mkoani Manyara, waliokuwa hawapati maji safi na salama kutokana na kutokuwa na miundombinu ya usambazaji wa maji ya uhakika wamefanikiwa kuondokana na adha hiyo baada ya mradi wa maji kuzinduliwa. Akisoma taarifa ya mradi huo wa maji jana kwenye mbio za mwenge wa uhuru, ofisa mtendaji wa kata ya Ayamohe John Tluway alisema mradi huo umegharimu sh388 milioni. 
 
Tluway alisema serikali kuu imechangia sh322 milioni, halmashauri ya mji sh19 milioni na serikali ya mtaa imechangia sh46 milioni kwa kutoa ardhi na kushiriki kwenye uchimbaji mtaro na ulazaji mabomba ya kilomita 15.
Alisema baada ya kukamilika kwa mradi huo wananchi wa eneo hilo hivi sasa watapata huduma ya maji tofauti na awali walikuwa wanatembea umbali wa kilomita mbili kufuata huduma hiyo. 
 
“Lengo la mradi ni kusogeza huduma ya maji karibu na na wananchi wa kata ya Ayamohe na mitaa ya jirani inayowazunguka ili kuondoa upungufu mkubwa wa maji unaosababishwa na ongezeko la wakazi,” alisema Tluway. 
Awali, mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga akisoma taarifa ya halmashauri ya mji wa Mbulu alisema mwenge wa uhuru utatembea miradi sita ya thamani ya sh1.1 bilioni. 
 
Mofuga alisema mwenge utafungua mradi wa maji Ayamohe, uzinduzi wa kikundi cha wanawake cha unenepeshaji ng’ombe na uzinduzi wa kiwanda cha usindikaji wa mikate na biskuti. Alisema pia utakagua shughuli za klabu ya wapinga rushwa shule ya sekondari Daudi, kuweka jiwe la msingi kituo cha afya Daudi ufunguzi wa vyumba vinne vya madarasa na choo cha wanafunzi na uzinduzi wa daraja la Endamaksi. 
 
Mmoja kati ya wakazi wa Ayamohe Jane Bayo alisema mradi huo wa maji utawanufaisha wananchi wa eneo hilo waliokuwa wanatembea umbali mrefu kwa ajili ya kufuata huduma hiyo. Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa kwa mwaka 2018 Charles Kabeho aliipongeza halmashauri ya mji huo kwa kutekeleza mradi huo kwani wamefanikiwa kumtwika mama ndo ya maji. 
 Askari upelelezi wa kituo cha polisi Mbulu, Gloria Nasson akielezea madhara ya matumizi ya dawa za kulevya huku akiwa ameshikilia bangi wakati mwenge wa uhuru ulipotembelea banda la polisi, kushoto ni Mkuu wa kituo cha polisi Mbulu, Amiry Mlemba.
IMG-20180920-WA0171
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, Charles Kabeho akitambulishwa kwa Mkurugenzi wa Mji wa Mbulu, Anna Mbogo na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Chelestino Mofuga. 
IMG-20180920-WA0069
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, Charles Kabeho akizungumza baada ya kuzindua kiwanda cha usindikaji wa mikate na biskuti kwenye mtaa wa Gwandumehi Halmashauri ya Mji wa Mbulu. 
IMG-20180920-WA0163
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Charles Kabeho akizindua kituo cha afya Daudi Halmashauri ya Mji wa Mbulu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...