Na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.

Naibu Waziri wa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiy amefungua wiki ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) pamoja na kuzindua nembo na kuzindua nembo mpya ya shirika hilo.

Akizungumza na waaandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mhandisi Nditiye amesema juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano kupitia ilani ya CCM katika sekta ya usafirishaji zitapelekea kuondoa kero mbalimbali na kukuza vipato vya wananchi 

Mhandisi Nditiye amesema hayo ili huhakikisha kauli mbiu ya uchumi wa viwanda inatekelezwa kwa ufanisi kwa kutumia miundombinu ya reli ya kisasa na uboreshaji wa reli ya kati kuelekea Dar -Isaka.Mhandisi amesema juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa wananchi wa Tanzania tushirikiane kwa pamoja kuunga mkono juhudi za serikali inayoongozwa na Mh.Rais Dkt.John Joseph Pombe Magufuli.

"Nawahakikishia kuwa serikali ya awamu ya tano itaendelea kuboresha huduma kwa wananchi na kuimarisha miundombinu ya reli na yenye lengo la kuleta manufaa na maendeleo ya Taifa la leo na kesho,"alisema Mhandisi Nditiye
Mwenyekiti wa bodi ta Wakurugenzi Shirika la Reli Tanzania (TRC),Profesa John Wajanga akizungumza waandishi wa habari katika ufunguzi wa wiki ya Shulilika la reli Tanzania leo hadi September 15 mwaka huu.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza leo na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa wiki ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kuwapongeza kwa nzuri na kusimamia vema shunguli za miradi mbalimbali inayoendelea ikiwemo wa ujenzi wa reli.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa bodi ta Wakurugenzi Shirika la Reli Tanzania (TRC),Profesa John Wajanga (picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii)
Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (wa tatu kushoto) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa wiki ya Shirika la reli Tanzania.
Meneja Uhusiano shirika la Reli Tanzania-TRC,Jamila Mbarouk akifafanua jambo katika ufunguzi wa shirika la Reli Tanzania.
Wafanyakazi wa shirika la Reli Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...