Waziri wa maji na umwaguliaji profesa Makame Mbarawa

Na Agness Francis,Globu ya jamii.
WAZIRI wa maji na umwaguliaji profesa Makame Mbarawa amewata wakazi waliojenga na wanaoishi Katika miundombinu ya mabomba ya maji hapa nchini kuondoka maramoja.

Profesa Mabrawa amesema hivyo ili kuweka usalama kwa wananchi hao kuondokana na adha ya kuhatarisha maisha ya wananchi hao.

Ameyasema hayo leo wakati akizungumza na vyombo vya habari  ofisini kwake Jijini Dar es Salaam kuwa  mwananchi atakaekaidi agizo hilo atachukuliwa hatua  kwa  kuwaondoa wote waliojenga katika miundo mbinu hiyo, kwa kuwa sheria iko wazi na inajulikana

Aidha Waziri Mbarawa amesema kuwa  serikali ya Tanzania kupitia shirika LA maji safi na maji taka  Dawasa itahakikisha zoezi hilo linafanikiwa katika kuhakikisha wananchi hao wanafata maagizo hayo bila kukiuka.

Hata hivyo Mbarawa amewataka wananchi wote  kuwa waangalifu katika kuzuia upotevu wa maji ambapo amesema mpaka kufika 2020  tatizo a maji  litakwisha na huduma ya upatikaniani wa maji itainhezeka u kuwafikia wanachi wote wa mijini na vijijini.

Ambapo ameahidi kubadilisha utendaji wa kazi hasa katika utekelezwaji wa wakandarasi  wasio na vigezo vya ufanyaji kazi kwa ufanisi pamoja na wasimamizi kulega lega katika usimamizi wa majukumu yao.

Vile vile profesa Mbarawa amezungumzia  utungwaji wa  Sheria Mpya ya maji kuwa italeta mapinduzi ya upatukanaji wa huduma ya maji nchini kote kwa urahisi.

"Wanachi wote wanaruhusiwa kutoa maoni  yao kuhusu sheria  hiyo mpya itakayotungwa,kwa Kuwa sheria hiyo haitakuwa ni yakwangu bali ni ya sisi wote"amesema profesa Mbarawa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...