Na Khadija Seif, Globu ya Jamii
KAMPUNI ya  kubashiri michezo nchini ya Sportspesa imezindua rasmi promosheni ya kuinua watu maisha yao hasa kiuchumi inayokwenda kwa jina la Shinda zaidi na Sportspesa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa Sportpesa, Tarimba Abbas amesema kampuni hiyo inaendesha shindano hilo kwa wateja wake ikiwa ni mara ya pili.

Ambapo kwa mwaka jana ilitoa takribani bajaj 100 kwa washindi kutoka mikoa mbalimbali nchini waliobuka washindi.

Pia Tarimba amesema  lengo la shindano hilo limejikita zaidi kwenye kubadilisha maisha ya Watanzania kwani washindi wamekua wakishinda zawadi mbalimbali ambazo kwa namna moja au nyingne zinawasaidia kujiongea kipato.

Ametoa rai kwa wateja kutumia fursa hiyo kubadilisha maisha yao kwani promosheni hiyo kila mmoja anayo nafasi ya kuwa mshindi na kufafanua shindano hilo linaambatana sana na wapenzi wa mpira wa miguu.

Kwa upande wa Submean Auto Limited Venkatesh Bussiness ambao ni wasambazaji wa Bajaji RE nchini  wametoa waranti kwa miezi 12 bajaj za watakaoshinda ili kuonesha imani kwa bidhaa hizo.

Pia wamewaomba watanzania kubashiri kupitia Sportpesa ili waweze kushinda hasa kwa kuzingatia kampuni hiyo inaongoza kwa  Afrika Mashariki.

 Wakati huohuo Meneja Uhusiano wa Sportspesa Sabrina Msuya  amefafanua jinsi ya kushiriki Kwenye promosheni ya Sindano hilo.

Msuya amesema kwa promosheni iliyopita ilifika mikoa 23 ya Tanzania na kwa kila aliyewekea ubashiri wake alipata nafasi ya kujishindia pesa taslimu,jezi na safari ya kwenda Uingereza ,Bajaji ni fursa peke kwa sasa kubashiri.
Meneja uhusiano wa shindano la shinda zaidi na Sportpesa, Sabrina Msuya (wa pili kulia) akizungumza na vyombo vya habarini kushoto ni Mkurugenzi wa utawala na udhibiti Abass Tarimba pamoja na wawakilishi kutoka klabu za mpira wa miguu nchini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...