Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, Mawaziri, Viongozi wa dini na Chama akivuta utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Daraja la Mto Sibiti lenye urefu wa mita 82 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 25 katika eneo la mto Sibiti Mpakani mwa Simiyu na Singida.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, Mawaziri, Viongozi wa dini na Chama akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mitambo itakayotumika katika mradi huo wa ujenzi wa Daraja la mto Sibiti.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Sibiti, Maswa na Singida katika eneo la mto Sibiti kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Daraja la Mto Sibiti lenye urefu wa mita 82 pamoja na barabara zake unganishi zenye urefu wa km 25.
 Wanachi mbalimbali kutoka Singida, Maswa, Sibiti wakishangilia wakati wa hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika eneo la Sibiti mpakani mwa mikoa ya Simiyu na Singida.
 Kikundi cha ngoma cha Lusanya kutoka Singida kikitumbuiza katika sherehe hizo.
Sehemu ya Daraja la mto Sibiti lenye urefu wa mita 82  upana mita 10.5 linalounganisha mikoa ya Simiyu na Singida kama linavyoonekana ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 70. PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...