Na Mwandishi Wetu Dodoma
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Njingu kusimamia kwa karibu Usajili na Uratibu wa NGOs nchini kwani kumekuwa na vitendo vya ovyo vinavyofanywa na NGOs.
Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Ikulu ya Chamwino Dodoma wakati akiwaapisha viongozi watatu aliowateua hivi karibuni akiwemo Mkurugenzi wa TAKUKURU Kamishna wa Polisi Diwani Athumani na Balozi wa Tanzania nchini Uganda Balozi Dkt Azizi Malima.
Dkt Magufuli amesisitiza kuwa NGOs zinatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria ambazo pamoja na mambo mengine zinayataka kuendesha shughuli zao kwa uwazi hususani katika masuala ya mapato na matumizi ya fedha za ufadhili wa shughuli zake.
“Nataka ukasimamie Usajili na Uratibu wa NGOs najua zipo chini ya Maendeleo ya Jamii kasimamie kuwe na uwazi wa utendaji kazi wa NGOs” alisisitiza Rais Magufuli.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu amemuhakikishia Rais Magufuli kutekeleza majukuu yake kwa akili, moyo na nguvu zake zote ili kufikia mafanikio anayoyatarajiwa na yanayotarajiwa na watanzania.
“Nikuahidi Mhe. Rais nitafanya kazi kwa nguvu na akili zangu zote kwa kushirikiana na wenzangu katika Wizara ili kuhakikisha mafanikio yanapatikana”alisema Dkt. Jingu.
Katibu
Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu
akipokea ua kutoka kwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mtoto Bi. Magreth
Mussai wakati alipowasili katika Oifisi za Wizara mara baada ya
kuapishwa kuwa Katibu Mkuu katika Ikulu ya Chamwino Dodoma.
Katibu
Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu
akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ( Idara Kuu Maendeleo ya Jamii) mara
baada ya kuapishwa kuwa Katibu Mkuu katika Ikulu ya Chamwino Dodoma.
Katibu
Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu
(kulia) akizungumza na wajumbe wa Menejimenti ya Idara Kuu Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mara baada ya kuwasili katika Ofisi za
Wizara baada ya kuapishwa kuwa Katibu Mkuu katika Ikulu ya Chamwino
Dodoma.
Mkurugenzi
wa Idara ya Usajili na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bw.
Marcel Katemba akitoa shukurani kwa niaba ya Menejimenti ya Idara Kuu
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Katibu Mkuu Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu mara baada ya kuwasili
katika Ofisi za Wizara baada ya kuapishwa kuwa Katibu Mkuu katika Ikulu
ya Chamwino Dodoma.
Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...