Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii.

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Mkonda ametoa mwezi mmoja sambamba  na kutopewa kazi nyingine kwa  Kampuni ya Nyanza hadi pale watakapomaliza miradi walioianza.Makonda ametoa kauli hiyo leo wakati akikagua miradi ya ujenzi wa barabara za halmashauri ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Amesema barabara hiyo yenye urefu wa kilomita moja inatakiwa kukamilika ndani ya miezi 15 lakini hadi sasa ni miezi 11 ujenzi hauridhishi."Mkataba uliosainiwa ni wa miezi 15 hadi sasa ni miezi 11 mradi unasuasu na hauridhishi" amesema Makonda

"Nnaagiza kwa halmashauri zote kampuni hii ya Nyanza isipewe kazi yoyote kwenye Mkoa wangu hadi watakapokamilisha miradi mitatu waliyoianza," ameongeza.Mkurgenzi wa manispaa ya Temeke Lusubilo Mwakabibi amesema kampuni imekuwa ikifanya kazi kwa kusuasua hivyo wajitathimini kwa kuwa kwenye halmashauri hiyo hawatapa nafasi.

"Nilipofika Temeke niliwaambia kwenye halmashauri yangu ujanjaujanja hakuna hivyo wajitafakari kwa kina kwani nnaweza kuvunja mkataba," amesema
 Mkuu wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari pamoja na kutoa agizo la mwezi mmoja kwa kampuni ya Ujenzi ya Nyanza kukamilisha  miradi ya ujenzi barabara ya Chang`o wilayani Temeke jijini Dar es salaam(Picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii)
 Mkuu wakoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda akiwa ameambata na mkuu wa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva, Mkurugenzi wa wilaya ya Temeke,Lusubilo Mwakabibi pamoja na Mkurugenzi wa Uzalishaji na Usambazaji wa Maji wa DAWASA, Mhadisi Aron Joseph wakikangua miradi mbalimbali inayojengwa na DMDP leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Uzalishaji na Usambazaji wa Maji wa DAWASA, Mhadisi Aron Joseph akifafanua jambo mbele ya Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika ziara ya kukangua miradi mbalimbali inayojengwa DMDP wilaya ya Temeke.

Mafundi wakiendelea na kazi ya ujenzi barabara 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA CHINI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...