NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MKUU wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi amewataka Madaktari wanaopatiwa mafunzo ya jinsi ya kufanya tathmini kwa mfanyakazi aliyeumia au kuugua mahala pa kazi, kutenda kazi kwa weledi na kwa haraka ili kuharakisha utoaji wa fidia.

Mkuu wa Mkoa alitoa rai hiyo leo Septemba 24, 2018 wakati akifungua mafunzo ya siku tano kwa madakatari na watoa huduma za afya kutoka mikoa ya Singida, Dodoma, Kigoma na Tabora kwenye chuo cha Uhasibu Singida.

“Katika kutoa fidia kwa mfanyakazi aliyepata madhara mahala pa kazi hakuna njoo kesho….njoo kesho, bali ni kumhudumia Mfanyakazi huyo kwa haraka ili aweze kupata fidia yake kutokana na madhara aliyoyapata kwa wakati na ninyi madaktari ndio wenye jukumu kubwa la kuhakikisha mnafanya kazi kwa weledi na kwa haraka.” Alisema.

Dkt. Nchimbi alisema, katika suala la utoaji fidia, Madaktari ni sawa na mahakimu, na wanayo dhamana kubwa sana kwani mapendekezo yao ndiyo yatatoa muongozo kwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, kuamua ni kiwango gani ambacho muathirika anapaswa kufidiwa au kutofidiwa kabisa.

“Kwa nafasi yenu Madaktari na kwa taaluma yenu mnafahamu sana namna ya kuwahudumia wahitaji wenu, lakini vile vile mnavyofanya katika tiba nyingine, huwezi kumtibu au kuwa na uhakika ni tiba ya namna gani mgonjwa anapaswa kupewa mpaka uwe na uelewa sahihi na ndio maana leo mko hapa ili muwe na uelewa sahihi, mtakapotoka hapa hatutarajii mseme sijui, sina uhakika, hayo siyo maneno ambayo tunataka yatoke kwenye vichwa vyenu baada ya mafunzo haya.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi, (aliyesimama), akitoa hotuba wakati akifungua mafunzo ya siku tano ya madaktari kutoka mikoa ya Singida, Dodoma, Tabora na Kigoma kuhusu namna ya kufanya tathmini ya Mfanyakazi aliyeumia au kuugua mahala pa kazi. Mafunzo hayo yameandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF). Wengine pichani kutoka kulia ni Daktari bingwa na mbobezi wa magonjwa ya mifupi kutoak MOI, Dkt. Robert Mhina, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskazi Muragila, na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini WCF, Dkt. Abdulsalaam Omary.
Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, akitoa neon la ukaribisho kwenye mafunzo hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi, (kushoto), akipeana mikono na Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, wakati wa mapunziko ya mafunzo hayo. Kulia ni Daktari bingwa wa magonjwa ya mifupa, na kionbgozi w atimu ya wataalamu wa kutoa mafunzo hayo, Dkt. Robert Mhina.
Dkt. Pascal Magessa kutoka Idara ya Madai na Tathmini WCF, akizungumza na mmoja wa washiriki.
Mgeni rasmi na meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na madaktari kutoka Singida.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...