Uongozi na watumishi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto ( Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto) tunaungana na
ndugu, jamaa na Watanzania wote katika kuombeleza msiba mzito kwa Taifa baada ya
ndugu zetu wapendwa kupoteza maisha katika ajali ya Kivuko cha Mv Nyerere
iliyotokea katika Ziwa Victoria, tarehe 20 Septemba, 2018.
Tunatoa pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe
Magufuli , ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na msiba huu na tunawaombea
majeruhi wote wapone haraka.
Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi. Amina.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
(Idara Kuu Maendeleo ya Jamii)
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
22/09/2018
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...