Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
LEO Septemba 11 dunia inakumbuka miaka 17 tangu kutokea kwa shambulio la kigaidi lililotekelezwa na kundi la kigaidi maarufu kama Al Queda dhidi ya Marekani kwa kulipua miji miwili na kusababisha mauaji na hasara kubwa.

Shambulio hilo ni moja kati ya mashambulio manne makubwa kuwahi kutokea, na shambulio hilo linafahamika zaidi kama Septemba 11 lilotokea asubuhi ya siku ya jumanne ya tarehe 11/9/2001 ambapo magaidi hao waliteka ndege 4 na kuzitumia kama silaha kwa kuzigongesha kwenye majengo makubwa ya kibiashara (World Trade Centre) katika majiji Newyork na Washngton DC.

Shambulio hilo lililofanyika asubuhi ilisababisha vifo zaidi ya watu 2996, majeruhi zaidi ya 6,000 na hasara ya uharibifu uliokadiriwa kufikia dola za kimarekani bilioni 10 na baadaye wengi wakagundulika na kuwa na matatizo katika mifumo ya upumuaji na saratani.

Ndege tatu zilifanikiwa kugonga majengo makubwa ya kibiashara na ndege moja ilitwaliwa na abiria na ikaangua katika mji wa Pennsylvania na magaidi 19 wa shambulio hilo walifariki.

Baada ya shambulio  Marekani walilaani shambulio hilo  na kuanza vita dhidi ya ugaidi ambapo kiongozi na mwanzilishi wa kundi hilo la Al Queda Osama Bin Laden alikimbilia nchini Afghanistan na kujificha.

Baada ya kumsaka gaidi huyo kwa miaka 10, Bin Laden aliuawa na jeshi la wana maji la Kimarekani mnamo 5/2/2011.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...