Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh. Jerry Muro amewashukuru wananchi wote wa Wilaya ya Arumeru kwa kujitokeza kwa wingi wakati wa ziara ya Mbio za Mwenge Kitaifa 2018 ambapo Wilaya ya Arumeru ilipokea Mwenge Kuanzia  Tarehe 16/09/2018 na Kuukabidhi Kwa Wilaya ya ARUSHA Mjini Siku ya Jumanne tarehe 18/09/2018 .

Dc Muro Amewashukuru Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Arumeru pamoja na kuwashukuru Wakurugenzi, Watumishi wa Halmashauri Mbili Za Arusha Dc na Meru Dc ambazo ziko Wilaya ya Arumeru pamoja na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM na Vyama Rafiki vya Siasa ambavyo Vilijitokeza na Kuunga Mkono mbio ZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa ambao umezindua na Kuweka Mawe ya Msingi ya Miradi mbalimbali ya Maendeleo yenye Thamani ya Zaidi ya Shilingi Bilioni 19 Kwa Mwaka 2018.

Dc Muro Mara ya Baada ya kuukabidhi Mwenge wa Uhuru Kwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe Gabriel Daqarro Amewashukuru Sana Viongozi wa Mbio Za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ambapo amesema Mbio ZA Mwenge wa Uhuru Kwa 2018 Zimekuwa tofauti kuliko miaka Mingine Kutokana na Umakini,Umahiri na Uweledi wa Wakimbiza Mwenge Wakiongozwa na Ndugu Charles Francis Kabeho ambao wamesaidia katika Kurudisha Heshima na thamani ya Mwenge wa Uhuru Kwa Kukagua na kutoa Maelekezo ambayo yamesaidia kuongeza umakini katika kusimamia Miradi ya Maendeleo pamoja na Fedha zinazotoka Serikali.

#ArumeruYetu #MwengeWetu #WakatiWetu

*Imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Arusha Tanzania *

19/09/2018
Pichani kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh. Jerry Muro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...