NA RIPOTA WETU,KILOMBERO
MAMLAKA
ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), katika kipindi cha mwaka 2017/18
imekamata baiskeli 60 za watuhumiwa wa ujangiri zikiwamo Nyaya zaidi ya
100 ndani ya Pori la Akiba Selous Kanda ya Kaskazini Magharibi- Msolwa.
Mkuu
wa Kanda hiyo, Augustine Ngimilanga alisema pamoja na kukamata nyenzo
hizo askari wa doria pia walikamata watuhumiwa wa ujangiri
waliofunguliwa kesi 92 zinazoendelea Mahakama ya wilaya ya Kilombero
mkoani Morogoro.
“Watuhumiwa
18 wameshasomewa kesi zao na kuhukumiwa baadhi wamefungwa miaka mitatu
na wengine miaka tisa jela,” alisema Ngimilanga na kuongeza:
“Tumeweka
mkakati wa kuhakikisha maeneo yote yanakuwa na ulinzi wa doria muda
wote, hii ni pamoja na kukabiliana nao kabla hawajaingia na kufanya
uharibifu,” alisema.
Mofisa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), katika Pori la Akiba Selous Kanda ya Kaskazini Magharibi -Msolwa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi na Kijiji cha Msolwa Station Kilombero mkoani Morogoro mara baada ya kutembelea Shule ya Msingi Ukombozi kujionea mchango wa uhifadhi kutoka kampuni za uwindaji wa kitalii.
Afisa Habari na Mawasiliano wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA),Twaha Twaibu kushoto akiwa na Mkuu wa Kanda ya Kaskazini Magharibi-Msolwa Pori la Akiba Selous Augustine Ngimilanga wakiangalia baiskeli zilizotumiwa na majangiri kubebea wanyamapori.
Mofisa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), katika Pori la Akiba Selous Kanda ya Kaskazini Magharibi -Msolwa wakiwa katika picha ya na viongozi na Kijiji cha Msolwa Station Kilombero mkoani Morogoro baada ya kutembelea jengo la Ofisi ya Kijiji cha Msolwa Station linalojengwa kwa fedha kutoka kampuni za uwindaji wa kitalii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...