*Ni kwa ajili ya washindi wa Tulia Traditional Dances Festival
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
MKURUGENZI wa Taasisi ya Tulia Trust Dk.Tulia Akson ameushukuru Ubalozi wa China nchini Tanzania kwa kumkabidhi pikipiki 10 kwa ajili ya washindi watakaopatikana kwenye tamasha la Tulia Traditional Dances Festival 2018.
Dk.Tulia ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge amekabidhiwa pikipiki hizo leo katika ubalozi huo na Mwakilishi wa Balozi wa China Tanzania nchini Xu Chen.Thamani ya pikipiki hizo ni Sh.milioni 21,600,000.
Akizungumza baada ya kupokea pikipiki hizo Dk.Tulia amesema anaushukuru ubalozi huo kwa kutoa zawadi hizo kwa ajili ya washindi wa tamasha hilo litakalofanyika kuanzia Septemba 18 hadi Septemba 22 mkoani Mbeya.
“Kwa niaba ya Taasisi ya Tulia Trust tunatoa shukrani zetu kwa ubalozi wa China nchini Tanzania kwa namna ambavyo wamekuwa pamoja nasi kwa kutoa zawadi kwa ajili ya washindi.
“Mwaka jana walitoa pikipiki 10 ambazo tulikabidhi kwa washindi.Lengo la tamasha hili ni kukuza utamaduni wetu na tumeanza na ngoma za asili.Pia tunataka wanaoshiriki pia wajikwamue kiuchumi,”amesema Dk.Akson.
Akifafanua zaidi kuhusu zawadi kwa washindi Dk.Askon amesema mshindi wa kwanza kwa idadi iliyopo watapata zawadi na kwamba jumla ya vikundi 108 vitashiriki.
Pia amesema tamasha hilo ni endelevu na linafanyika kwa mara ya tatu mfululizo na lengo kuu ni kukuza utamaduni wetu, pia iwe sehemu ya kuwawezesha wananchi kujenga uchumi,”amesema.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akipokea hati ya makabidhiano
ya zawadi ya Pikipiki 10 kutoka kwa Kaimu Balozi wa China nchini
Tanzania, Xu Chen, wakati wa hafla fupi iliyofanyika Ubalozi wa China
jijini Dar es Salaam, jana. Pikipiki hizo zitatolewa kwa washindi wa
kwanza 10 kutoka katika kila kundi kwenye Tamasha la Tulia Traditional
Dances Festival 2018 linalotarajia kuanza Septemba 18 hadi 22 jijini
Mbeya.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akisainiana hati ya
makabidhiano ya zawadi ya Pikipiki 10 na Kaimu Balozi wa China nchini
Tanzania, Xu Chen, wakati wa hafla fupi iliyofanyika Ubalozini hapo
jijini Dar es Salaam, jana. Pikipiki hizo zitatolewa kwa washindi wa
kwanza 10 kutoka katika kila kundi kwenye Tamasha la Tulia Traditional
Dances Festival 2018 linalotarajia kuanza Septemba 18 hadi 22 jini
Mbeya.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akizungumza na Kaimu Balozi wa
China nchini Tanzania, Xu Chen, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya
zawadi ya Pikipiki 10 kwa ajili ya washindi wa kwanza 10 kutoka katika
kila kundi kwenye Tamasha la Tulia Traditional Dances Festival 2018
linalotarajia kuanza Septemba 18 hadi 22 jijini Mbeya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...