Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Jeshi la Polisi mkoani hapa limesema litaendelea kuimarisha ulinzi katika uchaguzi mdogo wa marudio wa kugombea kiti cha ubunge unaotarajiwa kufanyika kesho Jumapili wilayani Monduli kama jinsi ilivyokuwa kwenye kampeni.

Akitoa taarifa hiyo leo asubuhi, Kamanda wa Polisi mkoani hapa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi, alisema wananchi wenye sifa za kupiga kura wajitokeze kwa wingi katika vituo vya kupigia kura kwani Jeshi hilo limezidi kuimarisha ulinzi ili uchaguzi huo ufanyike kwa amani na utulivu.

“Kama ilivyo kwenye kampeni hali ilikuwa tulivu na wakati wa uchaguzi tutahakikisha kwamba hali hii inaendelea kuwa shwari, askari toka vikosi mbalimbali watakuwepo wilayani hapo kwa ajili ya kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika hali ya usalama.” Alilisitiza Kamanda Ng’anzi.

Aidha aliwataka wananchi wa jimbo la Monduli mara baada ya kutimiza haki yao msingi ya kupiga kura wasikae kwenye vituo kwani hali hiyo inaweza kusababisha vurugu.

Kamanda Ng’anzi aliwaonya baadhi ya watu wanaopanga kufanya fujo wakati wa uchaguzi au mara baada ya uchaguzi kumalizika watakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria na kusisitiza kuwa yeye mwenyewe atakuwepo wilayani humo kwa ajili ya kujionea na kusimamia kwa karibu shughuli za Usalama katika kipindi chote cha kupiga kura hadi kutangaza matokeo.

“Ole wao watakaopanga kufanya vurugu, Jeshi la Polisi lipo imara na halitashindwa kumkamata yeyote atakayeshawishi au kufanya fujo katika uchaguzi huo ambao tunategemea utakuwa wa amani na utulivu”. Alimalizia kwa kuonya Kamanda Ng’anzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...