Na Grace Semfuko- MAELEZO.

Ujenzi wa jengo la tatu la abiria katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar Es Salaam (Terminal 3) umekamilika kwa asilimia 81, na miezi minane ijayo kazi zote za ujenzi wa majengo na mahitaji yote ya uwanja yatakuwa yamekamiliki na tayari usafiri wa anga wa Tanzania kukidhi mahitaji yote ya kisasa kimataifa.

Ujenzi huo unaojengwa na kampuni ya Bam International ya Uholanzi ikisaidiwa na kampuni zingine 21 za kihandisi za ndani na nje ya nchi, ujenzi ulianza Juni mwaka 2013 na utakamilishwa Mei 31, 2019 kwa gharama Yuro 254 milioni, sawa na shilingi Bilioni 560 za kitanzania.

Akizungumza uwanjani hapo Msimamizi wa Jengo hilo kwa upande wa Mradi huo kutoka Wakala wa Taifa wa Barabara TANROADS, Mhandisi Burton Komba, amesema ujenzi huo unaendelea vizuri na kwamba kukamilika kwake kutarahisisha kusafirisha Abiria wa Kimataifa ambao kwa sasa wanahudumiwa na Uwanja huo jengo la pili (Terminal 2).

“Uwanja wa Ndege wa Kimataifa jengo la tatu utakamilika mei 31 mwakani ambapo utahudumia Abiria milioni 6 kwa mwaka,hii itasaidia kuhudumia abiria wengi zaidi ambao walikuwa wakihudumiwa na Terminal 2, (jengo la pili)”.

Kukamilika kwa uwanja huu wa jengo la tatu ambapo huduma zote zimewekwa katika viwango vya juu vya kimataifa na hivyo jengo hilo kutumika kutoa huduma za viwango vya kundi la watu muhimu (VIP) na watu mashuhuri kibiashara (CIP).

Mhandisi amesema wakati jengo la pili linajengwa lengo lilikuwa ni kuweza kumudu abiria milioni moja na nusu lakini akasewma kwa sasa jengo limekuwa likihudumia zaidi ya idadi hiyo, “tumekuwa tukifikia abiria milioni mbili na nusu” alisema Mhandisi Komba.

Jengo hilo la tatu litakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege 17 hadi 19 zikiwemo ndege kubwa kwa wakati mmoja na hivyo kumudu abiria hadi milioni 6 kwa mwaka, pia eneo la nje ya uwanja kuna nafasi ya kuegesha magari 2,000 kwa dhamira ya kushusha na kupakia abiria wanaokuja na kuondoka nchini.

Kukamilika kwa ujenzi huo ni juhudi za serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha miundombinu inaboreshwa, lengo likiwa ni kufanikisha usafiri wa anga kasasa zaidi ili kuleta tija kwa uchumi wa Tanzania toka abiria na mizigo ya ndani na mataifa mbalimbali duniani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...