UONGOZI wa Halimashauri ya Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro umeonyesha kuridhishwa kwake na namna Mradi wa Kilimo Hifadhi unaotekelezwa wilayani humo na Baraza la Kilimo Tanzania (ACT) chini ya Mradi wake wa Ubia wa Kilimo Tanzania ulivyoweza kuwasaidia wakulima kwa kupata mavuno mengi ukilinganisha na hapo awali. 

Kauli hiyo imetolewa Jana na Kaimu Mkurugenzi wa halimashauri hiyo John Nnko,Wakati alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Baraza la Kilimo Tanzania (ACT) waliofika wilayani humo kujionea utekelezaji wa Mradi wa kilimo Hifadhi unaotekelezwa na Baraza la Kilimo Tanzania chini ya Mradi wake wa Ubia wa Kilimo Tanzania.

Alisema kuwa mpaka sasa kumekuwa na mwikitio mkubwa wa wakulima kutaka kujifunza zaidi namna ya kulima kilimo hifadhi hasa katika mazao ya mahindi na maharage ambapo alilishukuru Baraza la Kilimo kwa kutekeleza Mradi huo wilayani Same ambao unawafanya kupata mavuno mengi na kutokuwa na hofu ya ukame.

“Mpaka sasa Mradi huu wa Kilimo Hifadhi umekwisha kuwafikia zaidi ya wakulima 1,300 na uko katika vijiji tisa pekee, lakini tunaona mwitikio wa wakulima unazidi kuwa mkubwa wa kutaka kujua namna ya kulima kwa kutumia teknolojia hii, kwakweli ACT tunawashukuru sana kwa sababu pia hata watalaamu mmetuletea nyie” Alisema.

Miongoni mwa vijiji vinavyotekeleza mradi huo wilayani humo ni pamoja na Saweni, Hedaru,Kisiwani, Njiro, Mpirani na Ishinde ambapo wakulima waliueleza ujumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya ACT iliyofika katika mashamba yao kuwa tangu mradi huo wa Kilimo hifadhi ulipoanza mwaka 2011 vipato vyao vimeimarika huku gharama za uandaaji wa mashamba zikipungua.

Bw. Paul Mtango ambaye ni Mkulima wa Kijiji cha Mpirani Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro akiwaonyesha Wajumbe wa Bodi ya Baraza la Kilimo Tanzania (ACT) mfumo alioutumia kupanda Maharage katika shamba lake kwa kutumia Kilimo hifadhi, mfumo unaowafanya wakulima kupata mazao mengi tofauti na walivyokuwa wakilima awali.
Bw. Paul Mtango ambaye ni Mkulima wa Kijiji cha Mpirani Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Bodi ya Baraza la Kilimo Tanzania waliofika shambani kwake kujionea namna anavyonufaika na mradi wa kilimo hifadhi unaoratibiwa na ACT/TAP ambapo amewaeleza kwa kutumia Kilimo Hifadhi anaweza kupata gunia 12 za maharage kwa heka moja tofauti na awali alipokuwa akipata gunia 3 kwa hekari..
Bw. Paul Mtango ambaye ni Mkulima wa Kijiji cha Mpirani Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro akisisitiza jambo kwa Wajumbe wa Bodi ya Baraza la Kilimo Tanzania (ACT) waliofika shambani kwake kujionea namna anavyonufaika na mradi wa kilimo hifadhi unaoratibiwa na ACT/TAP, kuhusu namna kilimo hifadhi kinavyohifadhi ardhi vizuri kwa kizazi kijacho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...