Na Emmanuel Massaka,Global ya jamii
WILAYA ya Mkuranga ni moja ya wilaya saba zilizopo mkoani pwani wakazi wake  wakijishughuisha sana na shughuli za kilimo ilikujipatia kipato.

Wilaya ya Mkuranga inalima mazao  mbalimbali ya biashara na ya chakula ikiwemo Mihogo,Mbaazi,Korosho Machungwa Ufuta Mananasi pamoja na Nazi.

Pia wananchi wa Mkuranga wanategemea sana kilimo katika uchumi wao ambapo moja ya zao lililoshika kasi ni korosho,wanasomesha watoto kupitia korosho pamoja na kukuza pato la mtu mmoja mmoja.

Akizungumza wilayani Mkuranga mkoani Pwani Umri  Manage  mkulima wa mihogo na bamia alisema kuwa  kilimo kimemsaidia kwani ndio kinachoendesha Maisha yake"mimi nalima bamia linaniongezea kipato changu cha kila siku pia namsaidia mume wangu baadhi ya majukumu"amesema.

Manage  alitoa wito kwa wanawake wote nchini kuacha kujibweteka na kuacha utegemezi masala yake wajishughulishe katika shughuli mbalimbali za maendeleo.
 Mfanyabiashara na Mkulima wa Bamia,Umri Manage akizungumza na Michuzi Blog kuhusiana Kilimo.Wananchi wakivuna Mihogo   kama walivyokutwa na kamera yetu

Wananchi  wa wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani wakivuna Mihogo   kama walivyokutwa na kamera yetu.
Picha na Emmaniel Massaka wa Global ya jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...