Na Mwandishi wetu
IMEELEZWA kuwa katika mazingira ya sasa ya kuipeleka Tanzania katika uchumi wa kati kwa kuwa na viwanda ni lazima taifa litakuwa na mabadiliko katika makazi na kwamba miji mingi itachipuka.
Aidha serikali inapotekeleza mpango wake wa pili wa maendeleo  2016/17-2020/21 katika mpango wa muda mrefu wa maendeleo kwa lengo la kuwezesha mabadiliko ya kiuchumi kwa maendeleo ya watu uwepo wa miji ni wa lazima.
Aidha mazingira duni ya maisha katika vijiji kunafanya watu kuhamia katika maeneo yenye shughuli mbalimbali na hivyo kukuza miji iliyopo.
Hayo yalisemwa na Dk Lorah Basolile Madete, Mchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Fedha kwenye mkutano wa mkutano wa 5 wa jukwaa la ukuaji wa miji Tanzania (Tanzania Urbanisation Laboratory - TULab) ulioambatana na uwasilishaji wa tafiti tatu zilizofanywa na TUlab kuanzia mwaka jana.
Pia alisema tofauti kubwa ya kipato iliyopo vijijini na mijini inafanya maeneo ya jirani na vijiji kubadilika na kuanza kuchukua muonekano wa miji.
“Ndio kusema ni lazima kujiandaa kwa mabadiliko hayo na kuwa na  mpangilio wa kudhibiti ukuaji wa miji, kinyume chake Tanzania haitaweza kuvuna faida katika uchumi, kijamii na kimazingira kama miji itakua ghafla bila mipango mathubuti” alisema Dk Madete.
Katika mkutano huo ilielezwa kuwa kudhibiti miji ni kitu muhimu ikiwa mataifa yanataka kuwa na maendeleo endelevu ya kiuchumi na ustawi wa jamii.
Miji hiyo inatakiwa kupangwa na kukua kwa mujibu wa makubaliano ya dunia kama  yale ya Paris na maendeleo endelevu yaliyokubaliwa na Umoja wa Mataifa.
 Mkuu wa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF),  Bw. Deodatus Sagamiko akitoa neno la ukaribisho kwa niaba ya Mkurugenzi wa ESRF Dk Tausi Kida wakati wa Mkutano wa 5 wa maabara ya ukuaji wa miji Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
 Mchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Lorah Basolile Madete akitoa neno la ufunguzi wakati wa Mkutano wa 5 wa maabara ya ukuaji wa miji Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), jijini Dar es Salaam.
 Bw. Anton Cartwright wa Kituo cha Afrika cha miji kutoka nchini Afrika Kusini akiwasilisha Muhtasari wa tafiti tatu zilizofanyika chini ya Maabara inayoshughulikia mabadiliko kuelekea miji Tanzania (TULab)  na kuongoza majadiliano kuhusu athari za kisera katika tathmini ya kitaifa ya mabadiliko kuelekea miji (National Urbanization Transition Assessment -NUTA) wakati wa mkutano wa 5 wa maabara ya ukuaji wa miji Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), jijini Dar es Salaam.
 Mratibu wa Maabara inayoshughulikia mabadiliko kuelekea miji Tanzania (TULab) kutoka ESRF, Reshian W. Kanyatila akielezea masharti ya ushiriki katika shindano la utoaji huduma katika majiji.
 Mtafiti Msaidizi na Mratibu wa Miradi wa Chuo Kikuu cha Ardhi, Bw. Emmanuel Njavike (katikati) akiwasilisha waliyojadili katika kikundi kazi wakati wa mkutano wa 5 wa maabara ya ukuaji wa miji Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wakitoa maoni wakati wa mkutano wa 5 wa maabara ya ukuaji wa miji Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jana jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...