Na Tiganya Vicent
SERIKALI ya Wilaya ya Uyui imesema itawachukua hatua watumishi ambao hadi kufikia mwisho wa mwezi huu (Septemba) watakuwa bado hawajahamia katika eneo la Isikizya na kuacha kuishi Tabora mjini.

Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora(Uyui).

Alisema haiwezekani Halmashauri hiyo imenunua nyumba kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika eneo hilo lakini ni watumishi wachache ndio wanaoishi katika nyumba hizo na kuzifanya zile ambazo hazikaliwi kuanza kuchakaa.

Msuya aliongeza kuwa watumishi wamekuwa wakitumia gharama kubwa ya nauli ya kwenda na kurudi Tabora mjini kwa sababu ya nauli na wakati mwingine kuchelewa kazini.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema kitendo cha watumishi hao kukaa nje ya kituo chao cha kazi ni kosa na kinapunguza ufanisi katika kutoa huduma kwa wananchi ambao kodi zao ndio zinatumika kuwalipa mshahara.

Alisema itakapofika mwisho mwa Mwezi huu mtumishi yoyote ambaye ataendelea kukaa Tabora mjini atakuwa amekaidi na hatua dhidi yake zitachukuliwa kwa mujibu taratibu na Sheria za utumishi wa umma.

Msuya alisema kuwa mtumishi wa aina hiyo atahesabika kuwa nje ya kituo chake cha kazi bila taarifa za Mwajiri wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...