Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na watumishi wa Wizara yake (hawapo pichani), kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji kazi. Lugola aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii pamoja na changamoto zote zinazowakabili na atashirikiana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu (kushoto), wanatatua changamoto za watumishi hao. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhan Kailima. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha Veta, jijini Dodoma, leo.
Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo (mstari wa mbele) wakiwa na watumishi wengine wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakimsikiliza Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola (hayupo pichani), wakati alipokua akizungumza na watumishi hao kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa kuiongoza wizara hiyo. Katika hotuba yake, Lugola aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii, pia aliwahidi watumishi hao atashirikiana na Katibu Mkuu kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili katika utendaji wao. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha veta, jijini Dodoma, leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati), akiandika mafanikio na changamoto zilizokuwa zinatolewa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Issa Ng’imba (kulia), katika mkutano wa watumishi wa Wizara hiyo, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Veta, jijini Dodoma. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu, wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima na kushoto ni Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serkali na Afya (Tughe), tawi la Wizara, Obeid Mbaga.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akimsalimia Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu alipokua anawasili katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Veta, jijini Dodoma kwa ajili ya kuzungumza na watumishi wa wizara hiyo, leo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...