Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza
na watumishi wa Wizara yake (hawapo pichani), kuhusu masuala
mbalimbali ya utendaji kazi. Lugola aliwataka watumishi hao
kufanya kazi kwa bidii pamoja na changamoto zote zinazowakabili
na atashirikiana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali
Jacob Kingu (kushoto), wanatatua changamoto za watumishi hao.
Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhan Kailima.
Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha
Veta, jijini Dodoma, leo.
Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo (mstari wa mbele) wakiwa na
watumishi wengine wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
wakimsikiliza Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola (hayupo
pichani), wakati alipokua akizungumza na watumishi hao kwa
mara ya kwanza tangu alipoteuliwa kuiongoza wizara hiyo. Katika
hotuba yake, Lugola aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa
bidii, pia aliwahidi watumishi hao atashirikiana na Katibu Mkuu
kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili katika utendaji
wao. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo
cha veta, jijini Dodoma, leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati),
akiandika mafanikio na changamoto zilizokuwa zinatolewa na
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Issa Ng’imba (kulia),
katika mkutano wa watumishi wa Wizara hiyo, uliofanyika katika
ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Veta, jijini Dodoma. Wapili
kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob
Kingu, wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima na
kushoto ni Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serkali na Afya
(Tughe), tawi la Wizara, Obeid Mbaga.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto),
akimsalimia Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob
Kingu alipokua anawasili katika ukumbi wa mikutano wa Chuo
cha Veta, jijini Dodoma kwa ajili ya kuzungumza na watumishi wa
wizara hiyo, leo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...