Frank Mvungi- MAELEZO
MKUU wa mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge, ameongoza mkutano wa majadiliano ya Baraza la Biashara la mkoa huo ili kupitia na kuhakiki mwongozo wa majadiliano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ili usaidie kukuza ushiriki wa sekta binafsi na kuchochea ukuaji wa sekta zinatoa ajira kwa wananchi walio wengi kama kilimo.

Akizungumza na wajumbe wa baraza hilo  leo Jijini Dodoma  na wadau wengine, Dkt. Mahenge amesema kuwa, mkutano huu una lengo la kuhakiki mwongozo wa majadiliano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ngazi ya Mikoa na Wilaya.

“Tunategemea utakuwa rejea thabiti kwa viongozi na watendaji ambao wamekuwa wakibadilika mara kwa mara kutokana na uteuzi au chaguzi”. Alisisitiza Dkt. Mahenge

Akifafanua zaidi, mkuu huyo wa mkoa wa Dodoma amesema mkutano huo wa majadiliano una lengo la kuhakikisha ushiriki wa sekta binafsi unaongozeka ili kuchochea maendeleo ya mkoa na taifa.

Aliongeza kuwa, majadiliano hayo yatasaidia kutatua changamoto zinazojitokeza mara kwa mara ambazo zimekuwa zikifubaza upatikanaji wa fursa za kiuchumi na kijamii na yanategemewa kutoa ufumbuzi wa changamoto  hizo kwa kuzingatia maandalizi ya majadiliano, kanuni za majadiliano na utekelezaji baada ya majadiliano.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge akifungua  mkutano wa kuhakiki mwongozo wa majadiliano kati ya sekta ya umma na binafsi  uliofanyika leo Jijini Dodoma.
 Mhadhiri  kutoka  Chuo  kikuu  Mzumbe Prof. Honest   Ngowi akiwasilisha rasimu ya mwongozo wa majadiliano kati ya sekta ya umma na binafsi  wakati wa kikao cha kujadili muongozo  huo leo Jijini Dodoma.
 Sehemu ya wakuu wa Wilaya wa mkoa wa Dodoma wakifuatilia mkutano wa kuhakiki mwongozo wa majadiliano kati ya sekta ya umma na binafsi  uliofanyika leo Jijini Dodoma. 

(Picha zote na MAELEZO)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...