Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
BINTI wa kwanza wa aliyekuwa Rais wa Marekani George W. Bush, Barbara Pierce Bush (36) amefunga pingu za maisha na Craig Louis Coyne (37) ambaye ni mwandishi na mtunzi  wa filamu katika harusi ya siri iliyohusisha familia siku ya jumapili huko Maine.

Barbara aliongozwa na baba yake George W. Bush  wakati akiolewa na Craig katika harusi ndogo iliyofanyika nyumbani kwao Kennebunkport Maine, Bush alieleza furaha yao (yeye na mkewe Laura) baada ya binti  yao kufunga ndoa na kumtakia kila la heri.

Wawili hao hawakuweka mahusiano yao wazi na imekuwa harusi ya kuduwaza wengi kwani walionekana kama marafiki wa muda mrefu.

Barbara ameeleza kuwa angetamani uwepo wa bibi yake na hiyo ilikuwa  zawadi kwa bibi yake na wajina wake Barbara Bush aliyefariki mwezi Aprili mwaka huu akiwa na umri wa miaka 92.

Katika ukurasa wake wa instagram bi. Laura Bush ameandika kuwa "Ilikuwa siku ya furaha kwa bintiye Barbara kufunga ndoa na mpenzi wake Craig na wamemfurahia kuwa sehemu ya familia yao" ameandika Laura kwenye picha ya familia.
 Aliyekuwa Rais wa Marekan George W. Bush akimuongoza bintiye Barbara kwenda kufunga pingu za maisha na mpenzi wake wa siku nyingi Craig Coyne.
 Barbara Pierce Bush akiwa na mumewe Crag Louis Coyne mara baada ya kufunga ndoa siku ya jumapili huko Maine
 Picha ya familia 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...