Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, CHINA


Kansela wa Idara ya Habari, Wizara ya Mambo ya Nje katika Jamhuri ya Watu wa China, Bw. Gong Anmin amemuahidi Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dkt. Hassan Abbasi kushughulikia suala la mafunzo kwa Wanahabari wa Tanzania kwa lengo la kuwajengea uwezo katika sekta ya mawasiliano.

Bw.Gong ameyasema hayo wakati wa mkutano maalumu baina yake na ujumbe kutoka Tanzania ulioongozwa na Dkt. Abbasi uliolenga kujifunza na kubadilishana uzoefu katika sekta ya habari na mawasiliano na wataalamu wa Serikali ya China. Bw. Gong aliongeza kuwa: "suala la kuongeza uwezo kwa wanahabari ni muhimu kwani itasaidia kuongeza taaluma waliyonayo hivyo nitajitahidi kufanikisha mafunzo kwa wanahabari wa Tanzania ambayo ni nchi rafiki na China kwa miaka mingi"

Mbali na hayo Dkt. Abbasi pia amekutana na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje anayeshughulikia Idara ya Masuala ya Afrika Bw. WAN Li. Katika Mazungumzo yao Bw. Wan amesema kuwa urafiki wa Tanzania na China ni wa muda mrefu na ulianzishwa na waasisi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Mwenyekiti Mao Zedong hivyo kuahidi kutunza na kudumisha urafiki huo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...