Na Imma Msumba, Arumeru

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe.Jerry Muro amevitaka vyama vya siasa kuacha  malumbano na mvutano isiyokuwa na tija kwa wananchi wa Arumeru na badala yake amewataka kuungana na serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Arumeru.

Mh. Muro ameyasema hayo baada ya kuingilia kati mgogoro wa umiliki wa jengo ambalo awali lilikuwa likitumiwa na chama cha ushirika kata ya Ilikiurei hatua iliyosababisha kufungwa kwa ofisi ya serikali ambayo ilikuwa ikihudumia wananchi wa vitongoji viwili.

Kwa upande wao wananchi wanaoishi katika vitongoji hivyo mbali na kumpongeza Dc Muro kwa kuchukua hatua kwa haraka kuwa ofisi hizo zifunguliwe wamesema uamuzi huo utawasaidia kupata huduma ambazo wamekuwa wakizikosa kwa muda mrefu kutokana na mvutano wa umiliki wa jengo hilo kutoka kwenye vyama viwili vya siasa.

Baadhii ya Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe.Jerry Muro alipokuwa akizungumza nao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...