Na Said Mwishehe

MKUU wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro amesema wamekata silaha nne ikiwemo ya kivita ambayo inarisasi 19.

Sirro amesema hayo muda huu wakati anaendelea kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu tukio la kupatikana kwa Mfanyabiashara Mohammed Dewji 'MO'. Ametaja silaha hizo ni AK 47, bastola tatu na risasi 16 ambazo zilikuwa ndani ya gari iliyohusika kumteka MO.

Ameongeza kwamba hata hivyo watekaji hao walijaribu kuichoma moto gari hiyo kwa lengo la kupoteza ushahidi lakini ikashindikana .

IGP Sirro amesema uchunguzi unaendelea ili kubaini watekaji hao na kwamba kokote walioko watatafutwa na hatimaye wapatikane wakiwa hai au wamekufa .

Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi...endelea kufuatilia Michuzi Blog
KUU wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari katika viwanja vya Gymkana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...