Na Shushu Joel,Chalinze.
MBUNGE wa jimbo la chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani pwani Ridhiwani Kikwete ameipongeza Benk ya Nmb kwa juhudi zao za kutoa misaada kwa jamii ili kutatua changamoto mbalimbali zinazokuwa zikiwakabili wanajamii.

Akitoa pongezi hizo jana, katika kata ya kiwangwa alipokuwa akipokea vifaa mbalimbali vya hospital vilivyotolewa na benk hiyo,Ridhiwani alisema kuwa awali hospital hiyo ilikuwa na changamoto ya vitanda kwa ajili ya kinamama kuweza kujifungulia lakini kutokana na msaada huo tatizo hilo limebaki kuwa ni historia .

“Naipongeza benk ya Nmb kwa kutambua thamni ya kinamama wa chalinze ingawa katika nchi yetu kuna changamoto nyingi sehemu zingine lakini nyie mmeamua kutuletea misaada huu katika halmashauli yetu ya chalinze”Alisema Ridhiwani

“Mimi nawatia moyo tu kwa niaba ya wananchi wa chalinze msichoke kutusaidia kwani mahitaji yetu bado ni mengi ingawa nasi kama serikali tunapambana ili kuihakikisha kinamama wanajifungua bila matatizo ya aina yeyote hile ndio maana hata vifo vya kinamama chalinze wakiwa wanajifungua vinazidi kubaki kuwa historia”

Aliongeza kuwa awali walikuwa wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa viwanda kwa ajili ya kinamama kujifungulia katika hospital hiyo lakini Nmb imewapatia vitanda 10 kwa ajili ya kupunguza tatizo hilo hivyo amewataka wananchi wa kata hiyokwa kushirikiana na watumishi wa hospital hiyo kuhakikisha wanavilinda vifaa hivyo ili viweze kuwasaidia kwa kipindi kirefu.
 Mbunge wa jimbo la chalinze Ridhiwani Kikwete  akipokea vifaa vya wagonjwa kwa ajili ya hospital ya kiwangwa vilivyotolewa na benk ya Nmb
 Mbunge wa jimbo la chalinze Ridhiwani Kikwete  akipokea vifaa vya wagonjwa kwa ajili ya hospital ya kiwangwa vilivyotolewa na benk ya NMB.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...