NAODHA wa timu ya Taifa ya Mpira wa Kikapu chini ya Miaka 18 Jesca Ngisaise anatarajia kusafiri kesho alfajiri kuelekea Senegal kwenye majaribio.
Jesca amekuwa zao zuri la vijana katika mchezo wa kikapu nchini akionekana kufanya vizuri pale anapokuwa anapewa nafasi na kama atafanikiwa kufanya vizuri kwenye majaribio hayo atapata nafasi ya kujiunga na NBA ACADEMY.
Jesca amekuwa zao zuri la vijana katika mchezo wa kikapu nchini akionekana kufanya vizuri pale anapokuwa anapewa nafasi na kama atafanikiwa kufanya vizuri kwenye majaribio hayo atapata nafasi ya kujiunga na NBA ACADEMY.
Kama Jesca atafanikwia kujiunga na NBA Academy atakuwa amepiga hatua moja kubwa sana kuelekea kucheza kwenye WNBA nchini Marekani.
Jescar mwenye umri wa miaka 17 na amekua akifanya vizuri katika timu ya Taifa pia aliweza kuchagulia katika timu ya All Stars kwenye mafunzo maalumu ya BWB yaliyofanyika kule Africa kusini mwezi wa nane. Tunamtakia kila la heri aendelee kutuwakilisha vyema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...