*Hassan Dalali,wanachama watoa ya moyoni, wasema hivi..
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
UONGOZI wa Klabu ya Simba umeamua kufanya dua na kisomo maalumu kwa lengo la kumuomba Mwenyezi Mungu ili Mfadhili wao na mwanachama wa klabu hiyo Mohamed Dewji 'MO' apatikane akiwa salama.

Kisomo hicho kimefanyika leo mchana katika Makao Makuu ya Klabu ya Simba yaliyopo mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam ambapo mashabiki wa Simba wameshiriki kisomo hicho. Kabla ya kisomo wameelezwa wazi lengo lao kuu ni kumuomba Mwenyezimungu aweze kuleta wepesi kwenye matatizo yaliyompata Mlezi na Mwekezaji wao Mohamed Dewji 'MO' 

Kaimu Katibu Mkuu wa Klabu ya Simba Hamis Kisiwa amesema kuwa wamekusanyika kufanya dua leo hii wakiamini Mwenyezi Mungu ndio muweza wa kila jambo na hivyo huko aliko Mohammed Dewji apatikane na arudi akiwa salama.

Amesema hayo baada ya kufanyika dua na kisomo maalumu kwa lengo la kumuomba Mungu afanye wepesi kwa kuwezesha Mo kupatikana."Wana Simba tumefanya kisomo ilo Mo aachiweakiwa salama.Kwa mwanachama wa Simba na sio wa Simba wamekusanyika kufanya dua hiyo ili Mohamed aachiwe akiwa salama na ndio msingi wa dua yetu," amesema Kisiwa
Kusoma zaidi BOFYA HAPA.
Kaimu Katibu mkuu wa Klabu ya Simba Hamis Kisiwa wapili kushoto akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kufanya kisomo kumuombea Mlezi wa klabu hiyo Mohamed Dewji ambaye ametekwa jana Oktoba 11 hoteli ya collesium jijini Dar es Salaam.
 Wanachama wa Klabu ya Simba wakimsikiliza kaimu katibu mkuu wa klabu ya Simba Hamisi Kisiwa  jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kufanya kisomo kumuombea Mlezi wa klabu hiyo Mohamed Dewji ambaye ametekwa jana Oktoba 11 hoteli ya collesium jijini Dar es Salaam.
Wanachama wa Klabu ya Simba wanawake wakishiriki kwenye kisomo cha kumwombe Mlezi wa klabu hiyo jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...