MIAKA 19 BILA NYERERE
NYERERE NA RAIA WAKAKAMAVU WA TANZANIA

Wakinamama Wako Mbele Katika Ulinzi wa Taifa

Na Judith Mhina-MAELEZO
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kiongozi aliyeshirikisha kila Mtanzania katika kujenga ukakamavu na kuwa sehemu ya ulinzi wa Taifa.
Hayo yamethibitika pale aliposhirikisha watoto, vijana, viongozi, wanaume kwa wanawake wa nyumbani, wenye kazi rasmi za serikali Taasisi, Mashirika ya Umma na binafsi katika Jeshi la kujenga Taifa, Jeshi la Mgambo na Chipukizi.
Akifunga mafunzo ya Mgambo kwa watumishi na wakazi wa Ikulu tarehe 1 Juni 1973,  kwa kikosi kilichoongozwa na Mama Maria Nyerere Mwalimu Nyerere  amesema “ Tanzania ina wajibu wa kujenga taifa kakamavu na imara kwa ajili ya ulinzi binafsi,  wa mipaka yetu,  Taifa na kujenga afya bora”
Mwalimu alithubutu kumshirikisha Mama wa Taifa ambaye ni Mke wake mwenyewe ili apate  mafunzo ya mgambo, kwa kujumuika na watumishi na wakazi wa Ikulu eneo ambalo waliishi yeye na familia yake.
Mwalimu ni kiongozi ambaye kwa mtazamo wa kawaida kila mmoja anaona anawajihi ambao haupatikani kwa watu wenye wadhifa kama wake kwa asilimia kubwa. Kitendo cha kumpeleka Mke wa Rais (mke wake mwenyewe) kujifunza mbinu za ukakamavu na ulinzi ni kiashiria tosha kwake kuwa watanzania wote ni sawa na anawapenda Watanzania kama anavyojipenda mwenyewe.
Hapa tunapata funzo ambalo Mwalimu Nyerere ametuthibitishia suala la kuwa mkakamavu ni la msingi hata ukiwa Mama wa nyumbani. Pia, ni sehemu ya kulinda afya yako ya mwili. Ukakamavu huo utakufanya kuwa mtu wa kufanya kazi na kuijifunza familia yako iwe sehemu ya mazoezi matokeo yake, ni familia yenye afya na kupunguzwa magonjwa yasiyoambukiza.
 Rais Nyerere akikagua jeshi la mgambo kwenye sherehe ya kumaliza mafunzo yao Juni 01, 1973 Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mwanamgambo Bibi Maria Nyerere akiwa tayari kuamrisha wanamgambo wenzake kwenye sherehe ya kumaliza mafunzo yao Juni 01, 1973 Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Wanamgambo wakipita mbele ya Rais Nyerere wakati wa sherehe ya kumaliza mafunzi ya mgambo Juni 01, 1973.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...