Girl Guides wa Wilaya ya Temeke, wakikataa ndoa na mimba za utotoni wakati wa maadhimisho a Siku ya Mtoto wa Kike yaliyoandaliwa na uongozi wa TGGA Temeke, kwenye Ukumbi wa Idd Nyundo Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam. Katikati aliyevaa miwani ni Mgeni rasmi Mwalimu Hawa Chanafi wa Shule ya Tandika. Chanafi alimwakilisha Meya wa Temeke.
TGGA Temeke hadi sasa ina wanachama 5200. Tamasha hilo lilihudhuriwa na wanafunzi kutoka shule za Wailes, Likwati, Keko Magurumbasi, Tandika, Chamazi na Uwanja wa Ndege.
Girl Guides wakiwa na bango lenye ujumbe wa Nguvu ya Mtoto wa Kike.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes wakiigiza kusikitika jinsi baadhi ya wanaume wanavyotoa vishawishi kwa watoto wa kike kwa lengo la kufanya nao ngono na kuwapatia mimba.
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya maadhimisho kumalizika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...