Na Karama Kenyunko, Glogu ya Jamii
MAHAKAMA imewaasa Majaji nchini kuzingatia sheria  zilizopo kulingana na mazingira ya Taifa na Jamii kwa ujumla katika mchakato mzima wa kutoa maamuzi ili kimuweza kutenda haki na usawa.

Wito huo umetolewa na majaji wastaafu wa Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi, jaji Rugazia, John Mjemmas na Agathon Nchimbi wakati wa hafla fupi ya kuwaaga kitaaluma iliyofanyika mapema leo Oktoba 19.2018  katika ukumbi wa wazi wa Mahakama Kuu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Jaji Nchimbi amewakumbusha majaji na mahakimu kuhakikisha kuwa  wanakuwa waaminifu wakati wanatimiza majukumu yao kama maofisa wa mahakama ili mwisho wa Siku kila mmoja aweze kuona haki imetendeka.

Amesema, kwa kuwa mahakama ni chombo cha kutoa haki basi ni muhimu kuzingatia sheria zilizopo kulingana na mazingira ya taifa na Jamii katika mchakato mzima wa kutoa haki, Maamuzi yawe ya haki na usawa siyo tu hivyo  bali yaonekane kuwa ya haki na usawa" Amesema Jaji Nchimbi.

Aidha amewaasa  majaji wa mahakama kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwataka wajielekeze katika kutenda haki, kwa mujibu wa viapo walivyoapa bila ya kuwa na uoga, upendeleo wala chuki.

Jaji Kiongozi Eliezer Feleshi, wa katikati,  wa pili kushoto ni Jaji mstaafu Agathon Nchimbi, wa pili kulia ni Jaji Gad Mjemmas, wa kwanza kulia ni Jaji wa mahakama kuu divesheni ya Arshi, jaji, Crensensia Makuru na kwa kwanza kushoto ni Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu divisheni ya ardhi, Rehema Kerefu wakiwa katika Picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa hafla hiyo
 Jaji kiongozi, Eliezer Feleshi wa katikati waliokaa akiwa katika Picha ya pamoja na majaji wastaafu wa Mahakama Kuu kitengo cha ardhi, na Watumishi wengine wa Mahakama Kuu mara baada ya hafla ya kuwaaga kitaaluma iliyofanyika leo katika ukumbi wa wazi  wa Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
 Jaji Kiongozi Eliezer Feleshi, wa katikati waliokaa, akiwa katika Picha ya pamoja na baadhi ya waandishi wa Habari walioshiriki katika hafla ya kuwaaga kitaaluma majaji waliostaafu,  wa pili kushoto ni Jaji mstaafu Agathon Nchimbi, wa pili kulia ni Jaji Gad Mjemmas, wa kwanza kulia ni Jaji wa mahakama kuu divesheni ya Arshi, jaji, Crensensia Makuru na kwa kwanza kushoto ni Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu divisheni ya ardhi, Rehema Kerefu. 
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...