WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema changamoto ya upatikanaji wa ajira hususani kwa vijana imeanza kupungua nchini baada ya viwanda vingi kuanza kufanya kazi.

Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kukuza uchumi kutoka wa chini hadi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo mwaka 2025.

Aliyasema hayo jana jioni (Jumamosi, Oktoba 6, 2018) alipotembelea kiwanda cha kukoboa kahawa cha BUKOP na cha kusindika kahawa cha Tanica, mjini Bukoba.Alisema kwa sasa tabia ya vijana wengi kukaa vijiweni imepungua kwenye maeneo mengi nchini baada ya wengi kuajiriwa katika viwanda mbalimbali vilivyoanzishwa na kufufuliwa.

Waziri Mkuu alisema viwanda vimekuwa vikitoa ajira nyingi kwa wananchi, ambapo alitolea mfano kiwanda kimoja cha Tanika kilichoajiri watumishi 800. “Nyie mlioajiriwa kiwandani hapa hakikishe mnafanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu na uadilifu wa hali ya juu ili kukiwezesha kiwanda kuendelea na uzalishaji,” alisisitiza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama kopo la kahawa wakati alipotembelea kiwanda cha kusindika kahawa cha TANICA kilichopo mjini Bukoba, Oktoba 6, 2018 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama paketi ya kahawa wakati alipotembelea kiwanda cha kusindika kahawa cha TANICA mjini Bukoba, Oktoba 6, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mtambo kusindika kahawa wakati alipotembelea kwanda cha kusindika kahawa cha TANICA mjini Bukoba, Oktoba 6, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha kukoboa kahawa cha BUKOP baada ya kutembelea kiwanda chao kilichopo mjini Bukoba, Oktoba 6, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali, Marco Elisha Gaguti. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi Mkuu wa kiwanda cha kukoboa kahawa cha BUKOP, Theobad Mushashu (katikati) kuhusu ukoboaji kahawa wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 6, 2018. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...