Maneno haya yamesemwa na Mama Maria Nyerere, Mke wa Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere mwasisi wa Taifa letu alipotembelewa na Viongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) TAIFA jana Oktoba 08/2018.
Viongozi hao kutoka Makao Makuu ya UVCCM ni Wakuu wa Idara Ndugu Hassan Bomboko (Uhamasishaji na Chipukizi), Peter Kasera (Organaizesheni, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa), Khamana Juma Simba (Vyuo na Vyuo Vikuu)
Mama Maria Nyerere ameipongeza kazi kubwa inayofanywa na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli na amewaomba Viongozi wote nchini, Vijana na wananchi kumuunga mkono na kufanya juhudi kwenye maeneo yao ili kusaidia kuijenga Tanzania Mpya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...