Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

WANANCHI wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wameelezwa kuwa wana kila sababu za kuhakikisha wanakuwa na afya bora na salama, kwani afya ni muhimu na afya ni mtaji mkubwa katika maisha ya binadamu.

Pia wamehimizwa kupima afya zao kwa lengo la kutambua iwapo wamepatwa na maambukizi ya UKIMWI au laa, kwani kwa atakaepatwa na ugonjwa huo ataanza kutumia dawa ya ARV  na hivyo ataishi maisha marefu.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo wakati akizungumza na wananchi kuhusu kampeni inayoendelea ya  kupambana  na UKIMWI na kujenga jamii yenye uelewa na furaha.Kizigo amesema mbele ya wananchi kuwa Serikali ilianzisha kampeni ya Furaha Yangu iliyozinduliwa kitaifa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kwa Mkoa wa Ruvuma ilizinduliwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu Agosti  31 mwaka huu 2018

"Wilaya ya Namtumbo tumeendelea na kampeni hii ikiwa na lengo kuu la kuongeza kiwango cha upimaji wa VVU hasa kwa wanaume na wananchi kwa ujumla. Hadi juzi Oktoba 18 mwaka huu wa 2018 Wilaya ya Namtumbo walipima wanaume 873 na 16 walipatikana na VVU ambao kati yao 13 wameshaanza dozi (ARVs)," amesema.

Ameongeza kuwa Wilaya ya Namtumbo wameendeleza jitihada hizo kwa kuanzisha ligi ya mpira wa miguu iitwayo Laigwanani Supwr Cup ambapo Laigwanani ni neno la kimasai linalomaanisha Kijana na lengo ikiwa ni kuhamasisha vijana kujitokeza kupima, kujitambua afya zao na watakaokutwa na VVU kuanza dozi mapema.Mkuu huyo wa Wilaya amewaambia wananchi hao kwa watakaobainika kuwa na virusi vya UKIMWI dawa zipo na wataishi miaka mingi na kwamba anajua vijana wanaogopa kupima kwa kuhofia njia ambazo wamezipitia.

Amewashauri wananchi kujitokeza na kupima afya na watambue afya ni mtaji muhimu katika maisha na ndio maana wilaya ya Namtumbo imeona umuhimu wa kampeni hiyo ya kuhamasisha kupima UKIMWI ikaendelea na lengo ni kihakikisha afya za wananchi zinakuwa salama.Pia amewashauri kwa wale ambao hawapo ndani ya ndoa wawe waache kujihusisha na ngono zembe na wasubiri hadi watakapoingia kwenye ndoa au wawe na wakishindwa basi wawe na mpenzi mmoja na wawe wanatimia mpira ili kujikinga na maambukizi.

Kizigo ameongeza ni vema vijana wakatambua wao ni Taifa la leo na kesho na hivyo kujilinda kwa kuwa na afya njema ni jambo la msingi kwani wakiwa na afya njema watakuwa na fursa ya kujituma kwa ajili ya maendeleo yao ,wilaya,mkoa na taifa kwa ujumla.
 Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo akisalimiana na mmoja wa Marefa watakaokuwa wakichezesha Ligi hiyo ya mpira miguu iitwayo LAIGWANANI SUPER CUP, Lengo ikiwa ni kuhamasisha vijana kujitokeza kupima, kujitambua afya zao na watakaobainika kuwa na maambuziki ya VVU wataanza dozi mapema.

 Pichani Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo akisalimiana na baadhi wachezaji wa timu walioshiriki  ligi ya mpira wa miguu iitwayo LAIGWANANI SUPER CUP, Lengo la kuanzishwa kwa Ligi hiyo ni kuhamasisha vijana kujitokeza kupima, kujitambua afya zao na watakaobainika kuwa na maambuziki ya VVU wataanza dozi mapema.
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo akikabidhiwa taarifa kutoka kwa Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo,kabla ya kuanza kwa mchezo wa Ligi ya mpira wa Miguu  iitwayo LAIGWANANI SUPER CUP.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...