NA JOHN MAPEPELE, MARA

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amewataka viongozi wote wa serikali kuanzia ngazi za vijiji,wilaya kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa rasilimali za mifugo badala ya hali ilivyo sasa ya kuiacha ikitoroshwa kwenda nchi za nje kwa kuamini kwamba jukumu la ulinzi wa rasilimali hizo ni la Wizara ya Mifugo na Uvuvi peke yake na ikosesha serikali mapato.

Waziri Mpina ameyasema hayo wakati akizundua mnada wa mpakani wa Kimataifa wa Mifugo katika eneo la Kirumi Wilayani Butiama mkoani Mara ambapo ameagiza kufungwa kwa minada yote ya mifugo iliyofunguliwa kinyemela kwani imekuwa kichocheo cha upotevu wa mapato wa Serikali na kuonya wanaoanzisha minada hiyo bila kufuata taratibu zilizopo watachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa sheria.

Aidha amemuagiza Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel kuanza mara kuihakiki minada yote iliyopo nchini ili kuibaini ambayo imeanzishwa kinyume cha sheria iweze kufutwa.“wako watu wanafungua minada kila sehemu wanaamua tu wakati taratibu za ufunguzi wa minada wanazijua kabisa ya kwamba ni lazima wizara iridhie kufunguliwa kwa mnada huo”alisisitiza Waziri Mpina
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akikata utepe kufungua Mnada wa Kimataifa wa Mifugo Kirumi ulioko wilayani Butiama mkoani Mara juzi, wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima{kushoto},Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Annarose Nyamubi}kulia} na Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akifunua kitambaa katika jiwe la msingi la ufunguzi wa Mnada wa Kimataifa wa Mifugo Kirumi ulioko wilayani Butiama mkoani Mara juzi, wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima{kulia} na Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel }kushoto}.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina aliyenyanyua mkono akiwa na Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel (kulia kwake) wakati wa ufunguzi wa Mnada wa Kimataifa wa Mifugo Kirumi ulioko wilayani Butiama mkoani Mara juzi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...