Muanzilishi wa mtandao wa Elimu wa Tesea Abdul Mombokaleo amesema kuwa msingi wa kuanzishwa kwa mtandao wa Tesea ni kurahisisha upatikanaji wa marejeo(notes) kwa wanafunzi kujifunza na kupata elimu kwa kutumia teknolojia ya kisasa.

Amesema mtandao huu utakuwa na marejeo(notes) zote za kutosha na ambayo yame hakikiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania ili kusaidia wanafunzi kupata marejeo yanayotakiwa katika masomo yao.“mtandao huu hauchukui nafasi ya mwalimu bali utamsaidia mwalimu kuandaa masomo kwa urahisi kwani notes hizo zinafata mtaala wa serikali kwa kuwa na silabasi zote zinazotakiwa kwa mwanafunzi kujifunza awapo shuleni”. amesema Mombokaleo

Amesema mtandao huo unaopatika kupitia simu za smartphone,laptop,tablet na computer za mezani na unaweza kupakuliwa kiurahisi na mwanafunzi kijisali na kuanza kutumia mtandao kwa gharama nafuu,na kupata masomo yote ya biashara,sayansi na elimu za dini ya kiislamu na kikristo pamoja na mitihani iliyopita (pastpapers).

Kwa upande Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Mwenyekiti wa taifa wa wamiliki wa shule binafsi nchini Charles Totera, amesema kuwa elimu inatakiwa kumsaidia mtu kuweza kutatua matatizo yake bila kusubiri msaada kutoka kwa mtu mwingine kwa uwezo wake wa kufikiri kutokana na elimu aliyonayo.
  Muanzilishi wa TESEApp Abdul Mombokaleo, akionyesha Tablet ambayo mwanafunzi anaweza kutumia katika kusoma katika mtandao wa TESEA ikiwa tayari imewekwa mtandao maalumu wa masomo ya sekondari (Kidato 1 – 4) na (kidato 5 – 6) akiwa na Mwenyekiti wa Taifa wa wamiliki wa shule na vyuo binafsi nchini (TAMONGSCO) Ndugu Charles Totera katika uzinduzi wa TESEApp. 
Muanzilishi wa TESEApp Abdul Mombokaleo, akionyesha Tablet ambayo mwanafunzi anaweza kutumia katika kusoma katika mtandao wa TESEA ikiwa tayari imewekwa mtandao maalumu wa masomo ya sekondari (Kidato 1 – 4) na (kidato 5 – 6) akiwa na Mwenyekiti wa Taifa wa wamiliki wa shule na vyuo binafsi nchini (TAMONGSCO) Ndugu Charles Totera katika uzinduzi wa TESEApp.

Muanzilishi wa TESEApp Abdul Mombokaleo wa kulia akisalimiana na Mwenyekiti wa Taifa wa wamiliki wa shule na vyuo binafsi nchini (TAMONGSCO) Ndugu Charles Totera katika uzinduzi wa TESEApp.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...