Akiongoza shughuli hiyo ya kuaga mwili wa aliekua Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni Dkt.Julian Bujugo  iliyohudhuriwa pia na viongozi wa vyama na Serkali,  Mstahiki Meya wa Manispaa ya kinondoni  Mh.Benjamini Sitta amesema,  Kinondoni imepoteza mpiganaji, mpenda haki, mtetezi wa wanyonge,  na mzalendo. 
"Bujugo alikuwa mzalendo, alikuwa ni mtu aliyependa kuona mambo yanakwenda, wanyonge wanapata haki, hata siku ambayo usiku wake mauti inamkuta, Mh Bujugo alikuja ofisini kwangu mchana kwa swala la walemavu wa magomeni kuhusiana na ada ya usajili wa kikundi wanayotozwa", alisema  Meya Sitta.

Shughuli hii ya kuuaga mwili wa marehemu Julian Rushaigo Bujugo imehudhuriwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Ndg Aron Kagurumjuli, wakuu wa idara na vitengo, wananchi wa kata ya Magomeni, pamoja na viongozi wa vyama na serikali, akiwemo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Bi.Kate Kamba, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni Ndg. Harold Maruma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda, pamoja na Baraza la Madiwani la Manispaa ya Kinondoni.

Bwana ametoa, bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi Amen.

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda
akiongoza waombolezaji  kuaga mwili wa aliekua Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni  Dkt.Julian Bujugo leo katika viwanja nya Manispaa hiyo  jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Sylivia Magdalena Kamba akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lililobeba mwili wa aliekua  Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni Dkt.Julian Bujugo leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG)
 Meya  wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akitoa heshima ya mwisho mbele ya jeneza lililobeba mwili wa alikua Diwani wa Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni Dkt. Julian Bujugo  katika viwanja vya manispaa hiyo leo jijini Dar es Salaam.
 Madiwani  walioshiriki kuaga mwili wa aliekua Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni  Dkt. Julian Bujugo.
 Sehemu ya waombolezaji walioshiriki kuaga mwili wa aliekua Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni  Dkt. Julian Bujugo.
 Sehemu ya waombolezaji walioshiriki kuaga mwili wa aliekua Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni  Dkt. Julian Bujugo.
 Sehemu ya waombolezaji walioshiriki kuaga mwili wa aliekua Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni  Dkt. Julian Bujugo.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG)
Sehemu ya waombolezaji walioshiriki kuaga mwili wa aliekua Diwani Kata ya Magomeni Manispaa ya Kinondoni  Dkt. Julian Bujugo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...