SUALA la kujitambua na kutambua nini mahitaji yako ni moja ya chanzo cha mabadiliko yanayohitajika katika maisha, Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira-UNEP, Joyce Msuya amebainisha.

Alisema hayo akizungumza na wanawake mbalimbali waliofika kusikiliza historia yake na jinsi alivyoweza kumudu maisha ya mama, mke na mfanyakazi katika mashirika mbalimbali ya kimataifa na kupanda ngazi.
Aidha alisema pamoja na kujitambua mtu anatakiwa kufanya kazi kwa kuwajibika, kujisukuma zaidi katika kazi na kufanya maamuzi ya kushirikisha familia hasa patna.

Msuya ambaye alianza kazi ya UNEP mwaka huu mwezi wa nane baada ya kupitia Benki ya dunia na mashirika mengine kadhaa alisema mfumo wa Tanzania wa shule, malezi ndiyo iliyofanya kuunganisha nguvu, uwezo na ujasiri wa kuweza kufanya mambo ambayo yamemfanya kupata nafasi kubwa zaidi.

Alisema mfumo wa Tanzania wa maisha umekuwa msukukumo mkubwa kwake kwani  aliweza kuishi na watu tofauti na kuvumilia huku akitekeleza wajibu wake kwa kujiongeza zaidi.Alisema kutokana na juhuzi za wazazi wake katika kusimamia malezi aliweza kupata maarifa zaidi ya kuishi kwa kuhudhuria shule za umma za Forodhani, Jangwani na Weruweru kisha kuchukua mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT) Mafinga na kumalizia mafunzo hayo Mlalakua.

“Ukweli ni kuwa wazazi wangu walitaka tuishi maisha ya kawaida kama watanzania wengine ndiyo maana walinipeleka shule za bweni na kuhakikisha naenda jeshini. “ alisema Mkurugenzi huyo ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi.

Anasema malezi ya kujitegemea yamemfanya awe na uwezo wa kufanya bajeti hali ambayo ilimwezesha kuishi vyema Scotland na hata alipoenda kuchukua shahada yake ya pili nchini Canada.“Kusema ukweli  Baba na mama walinitengenezea mfumo mzuri wa kuishi hasa pale walipojenga na kunihimiza kufanya kazi na kusoma wakati nikiwa mdogo.” Alisema Msuya.
Anasema amevuka vigingi vingi hasa kwenye muwashawasha wa masomo lakini kama walivyo watu wote alifanya maamuzi makini kuzingatia ushauri na kile anachokipenda.

Akiulizwa nini hasa kinamsukuma, alisema kwamba familia ni kitu muhimu kwake na kwamba amefanya mambo mengi akiwa na familia yake kuanzia mume wake ambaye wamo katika ndoa kwa miaka 20 na kujaliwa kuwa na watoto wawili.
 Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira-UNEP, Bi. Joyce Msuya akizungumza viongozi wanawake vijana kwenye mdahalo ambapo aliutumia kuhamasisha wanawake wengine kujituma uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bi. Natalie Boucly. 
 Mkurugenzi wa uendeshaji wa Doctors’ Plaza, Bi. Sophia Byanaku akiuliza swali kwa Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira-UNEP, Bi. Joyce Msuya (hayupo pichani) wakati wa mdahalo maalum kwa viongozi wanawake vijana ambapo walipata fursa ya kuhamasishwa kujituma na kujitambua uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya viongozi wanawake vijana walioshiriki kwenye mdahalo ulioendeshwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira-UNEP, Bi. Joyce Msuya (hayupo pichani) ambapo aliutumia kuhamasisha wanawake wengine kujituma uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam
Baadhi ya viongozi wanawake vijana wakiuliza maswali kwa Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira-UNEP, Bi. Joyce Msuya (hayupo pichani) wakati wa mdahalo maalum uliotumika kuhamasisha wanawake wengine kujituma na kujitambua ambapo umefanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira-UNEP, Bi. Joyce Msuya katika picha ya pamoja na viongozi wanawake vijana mara baada ya kumalizika kwa mdahalo huo uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...