Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson leo ametembelea Benki ya CRDB na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, AbdulMajid Mussa Nsekela. 

Dkt. Tulia alisema dhumuni la Mkutano huo ni kumpongeza, Nsekela kwa uteuzi wake wa kuwa Mkurugenzi Mtendaji Mpya wa Benki ya CRDB na kufanya mazungumzo juu ya masuala mbalimbali ya kiuchumi na maendeleo.
 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki wa Benki ya CRDB, AbdulMajid Mussa Nsekela, walipokuwa wakizungumza ofisini kwake, Azikiwe jijini Dar es salaam.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson akifurahi jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki wa Benki ya CRDB, AbdulMajid Mussa Nsekela wakati alipokuwa akisaini kitabu cha wageni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...