Na Victor  Masangu, Chalinze
WANAWAKE  wa kijiji cha Mduma  kata Magindu  katika halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani  kwa sasa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kutokuwa na nishati ya umeme hivyo inawalazimu kupatiwa matibabu  kwa kutumia mwanga wa tochi au simu  pindi wanapokwenda kujifungua  katika zahanati ya Mduma  kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa maisha yao.

Wakizungumza   kijijini hapo  kuhusiana na changamoto inayowakabili wanawake hao wamesema   kwamba kwa sasa  wanapata shida kubwa wakati wa kujifungua hasa katika nyakati za usiku kutokana na kuwa na giza hivyo kuwapa wakati mgumu  wauguzi  pindi wanapotekeleza majukumu yao.

Aidha walisema  kwamba kwa kipindi kirefu katika zahanati hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbali mbali za upatikanaji wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa hivyo wameiomba serikali ya awamu ya tano kuingilia kati suala hilo kwa lengo la kuweza kuwafikishia nishati ya umeme ambayo itakuwa ni mkombozi katika utoaji wa huduma hasa katika nyakati za usiku.

Kwa upande wake mmoja wa wauguzi katika zahanati ya Mduma Neema Muhagama amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo ya kutokuwa na nishati ya umeme hivyo inawapelekea  wakati mwingine kutumia mwanga wa tochi  za simu katika kuwapatia matibabu wagonjwa hasa kwa upande wa wakinamama wajawazito pindi wanapohitaji kujifungua.
 Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu wa katikati ambaye pia ni Mbunge wa viti maalumu (CCM) kutoka Mkoa wa Pwani  akikabidhi msaada wa Solar Power  kwa baadhi ya wauguzi wa zahanati ya Mduma iliyopo kata ya Kibindu  katika halmashauri ya Chalinze iliyopo Wilayani Bagamoyo   kulia kwake ni muuguzi Neema Muhagama akipokea kwa niaba ya wenzake.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Naibu Waziri wa nishati Subila Mgalu wa kulia ambaye pia ni Mbunge wa viti maalumu (CCM) kutoka Mkoa wa Pwani akimkabidhi msaada wa Solar Power  Martha Kilimba ambaye ni mmoja wa wauguzi  katika zahanati ya Kwamsanja iliyopo kata ya Kibindu katika halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo kwa lengo la kuwasaidia wagonjwa ambao wamekuwa wakipata adha ya kutibiwa kwa kutumia mwanga wa tochi za simu.
Naibu waziri wa nishati Subira Mgalu kulia ambaye pia ni Mbunge wa viti maalumu (CCM) kutoka Mkoani Pwani akimkabidhi msaada wa Solar Power mmoja wa wauguzi katika zahanati   ya Kibindu iliyopo kata ya Kibindu katika halmashauri ya Chalinze iliyopo Wilayani Bagamoyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...