Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

WATUMISHI watano wa Wizara ya Kilimo na Chakula wamefariki dunia leo asubuhi baada ya gari waliyokuwa wakisafiria kupata ajali wilayani Manyoni mkoani Singida.
Taarifa ya Katibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo ambayo ameitoa leo kwa vyombo vya habari amesema kuwa Wizara yao imepatwa na msiba wa watumishi wake watano.
Amesema watumishi hao waliopata ajali leo asubuhi wilayanu Manyoni mkoani Singida, walipokuwa safarini kuelekea Mwanza kikazi.
Amewataja watumishi hao waliofariki ni Stella Ossano (39), Esta Mutatembwa (36), Abdallah Mushumbusi (53), Charles Somi na Erasto Mhina (43)
"Miili ya marehemu ipo njiani kuja Hospitali ya Mkoa wa Dodoma leo Oktoba 21, 2018. Mungu azilaze roho zao mahala pema peponi, Amina," amesema Katibu Mkuu kwenye wizara hiyo.
Baadhi ya wananchi wakitazama namna ajali hiyo ya gari yenye namba za Usajili STK 8925 ikiwa imepta ajali eneo la Njirii Manyoni. Ambapo Gari ndogo, ya Wizara ya Kilimo na Chakula, iliyokua imebeba Wataalam wane pamoja na Dereva Wote wamefariki papo hapo. Wanaume watatu, na wanawake wawili. Miili imehifadhiwa katika Hosptal ya Wilaya Manyoni. Mwenyezi Mungu Awarehemu
Baadhi ya Maofisa wa Polisi wakitazama gari yenye namba za Usajili STK 8925 ikiwa imepta ajali eneo la Njirii Manyoni. Ambapo Gari ndogo, ya Wizara ya Kilimo na Chakula, iliyokua imebeba Wataalam wane pamoja na Dereva Wote wamefariki papo hapo. Wanaume watatu, na wanawake wawili. Miili imehifadhiwa katika Hosptal ya Wilaya Manyoni. Mwenyezi Mungu Awarehemu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...