Shirika la Hifadhi ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii NSSF ni kati ya Tasisisi za serikali iliyoshiriki kwenye maonyesho ya wiki ya Taifa ya Vijana yanayofanyika katika viwanja vya Tangamano wilaya ya Tanga mjini Mkoani Tanga ambapo wananchi wameombwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye mpango wa hiari . 

Kaimu meneja wa mkoa waTanga Bi Aisha Nyemba amesema kuwa katika maonyesho haya wananchi wote wanaotaka kujiunga kwa hiari na kujiwekea akiba wanaweza kufanya hivyo na kwamba NSSF itawatambua na kuweka katika rekodi za wananchama wapya. 

“Ukija hapa katika banda letu utaweza kuandikishwa na kutambulika kwenye rekodi zetu hivyo ni fursa ya pekee kwa wananchama wapya kujiandikisha katika maonyesho haya”alisema bi Aisha. Bi Aisha amesema kuwa tangu maonyesho haya yaanze Oktoba 8 mwaka 2018 wananchi wengi wamejitokeza kujiandikisha na kupata elimu kuhusiana na umuhimu wa mafao ya NSSF na kuvutiwa hasa hasa katika eneo la matibabu bure. 

Wananchi wanaojiandikisha kwenye mpango wa hiari ni wale waliopo kwenye sekta isiyo rasmi kama vile waendesha bodaboda,mama lishe, wajasiriamali na wengine wengi. 

Maonyesho haya ya Taifa ya wiki ya vijana yaatafikia kilele oktoba 14 mwaka huu ambapo yataendana na sherehe za uzimaji wa mwenge kitaifa katika uwanja wa Mkwakwani.
Kaimu meneja wa mkoa NSSF mkoa wa Tanga bi Aisha Nyemba akitoa maelekezo kwa mkazi wa Tanga ,Yahaya Katubu alipofika kwenye banda la NSSF,wakati wa maonesho  wiki ya vijana yanayofanyika katika viwanja vya Tangamano mkoani Tanga
OFisa madai wa shirika la Taifa ya Hifadhi ya Jamii NSSF Athuman Bakari akitoa amelekezo kwa wananchi wa mkoa wa TANGA waliotembelea kwenye maonesho ya wiki ya kitaifa ya Vijana yanayofanyika katika viwanja vya Tangamano Tanga
Ofisa Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii NSSF Bi Aisha Sango akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea katika banda la NSSF kwenye maonesho ya wiki ya Kitaifa ya Vijana inayofanyoka katika viwanja vya Tangamano mkoani TANGA
Ofisa mikopo wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii NSSF Athuman Bakari akitoa maelekezo kwa wananchi waliofika kwenye viwanja vya Tangamano yanapofanyika maonyesho ya wiki ya vijana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...