Na Greyson Mwase, Katavi

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ameagiza Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Katavi, Mhandisi Giliard Luyoka, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Afisa Usalama wa Wilaya, na Mwakilishi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha wanakuwepo wakati wa ufungaji na ufunguaji wa lakiri (seal) kwenye madini ya dhahabu ili kudhibiti utoroshwaji wa madini kwenye migodi.

Ameyasema hayo leo tarehe 09 Oktoba, 2018 mara baada ya kumaliza ziara yake katika Mgodi Dhahabu wa Katavi & Kapufi uliopo katika eneo la Singililwa Wilayani Mpanda mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika mkoa huo yenye lengo la kukagua shughuli za uchimbaji wa madini, kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji wa madini.

Katika ziara yake Nyongo aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Salehe Mhando, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji wa Madini Mkoa wa Katavi (KATAREMA), William Mbongo, Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Katavi, Mhandisi Giliard Luyoka, Wataalam wa Madini, Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na waandishi wa habari.

Alisema kuwa, ni kosa kubwa la kisheria kwa Afisa Madini Mkazi kufunga au kufungua lakiri (seal) pasipo kushirikisha Mkuu wa Wilaya, vyombo vya ulinzi na usalama na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kusisitiza kuwa iwapo itagundulika Serikali haitasita kuchukua hatua kali za kisheria.


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) akiendelea na ziara katika Mgodi wa Dhahabu wa Katavi & Kapufi uliopo katika eneo la Singililwa Wilayani Mpanda mkoani Katavi. 
Mkaguzi wa Migodi kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Katavi, Paul Veran (kushoto) akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) kwenye eneo yanapohifadhiwa makinikia ya dhahabu katika Mgodi wa Dhahabu wa Katavi & Kapufi uliopo katika eneo la Singililwa Wilayani Mpanda mkoani Katavi. 
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa nne kulia) akikagua shughuli za uchenjuaji wa dhahabu zinazofanywa na wachimbaji wadogo katika machimbo ya dhahabu ya Mkwamba yaliyopo katika kijiji cha Kapanda Wilayani Mpanda mkoani Katavi. 
Sehemu ya wachimbaji wadogo katika machimbo ya dhahabu ya Mkwamba yaliyopo katika kijiji cha Kapanda Wilayani Mpanda mkoani Katavi wakifuatilia ufafanuzi uliokuwa unatolewa na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (hayupo pichani) katika machimbo hayo. 
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akifafanua jambo alipokuwa akizungumza na wachimbaji wadogo katika machimbo ya dhahabu ya Mkwamba yaliyopo katika kijiji cha Kapanda Wilayani Mpanda mkoani Katavi (hawapo pichani).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...