Serikali imejipanga kuhakikisha miradi ya maji hapa nchini inatekelezwa kwa kasi kubwa kwa majiji unafikia asilimia 95 ambapo miji ya wilaya asilimia 90 na vijijini kwa asilimia 85 ifikapo mwaka 2020 ambapo kwa jiji la Arusha inatekeleza mradi mkubwa wa maji utakaozalisha lita million 200 kwa siku kwa gharama ya billion 520. 

Aidha Serikali imepanga kutekeleza Mradi mkubwa wa maji hapa nchini utakogharimu kiasi cha Trilion 1.1 sawa na dola za kimarekani million 500 kwa watanzania wamesubiria maji hivyo watakaopata nafasi ya kusimamia mradi huu kuutekeza kwa ufanisi na kwa wakati. 

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea visima vya maji katika kijiji cha Levolosi kata ya Kimnyaki wilaya ya Arusha dc na kutiliana saini Waziri wa maji na umwagiliaji Prof.Makame Mbarawa amesema kuwa serikali itaendelea kuhakikisha miradi hiyo inaondoa adhaa ya maji kwa watanzania 

Amesema kuwa jiji la Arusha kwa sasa linazalisha maji lita million 45 kwa siku wakati mahitaji yanayotosheleza kwa siku ni lita million 94 ndio maana serikali ikaliona hilo na ikaandaa mradi mkubwa uakapo kamilika utazalisha lita million 200 kwa siku ambao utaondoa tatizo la maji kwa jiji la Arusha na kuwa historia. 

“Jiji la Arusha kwa sasa kuna upungufu mkubwa wa maji ambapo serikali inakuja na mradi huu mkubwa kwa kuchimba visima 56 tunajenga mfumo wa kusafisha maji na mfumo wa kusambaza maji na mfumo wa kusafisha maji taka na wakandarasi wapo kazini”alisema Prof.Mbarawa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...