Na Frankius Cleophace Tarime.

Serikali imeombwa kuchukua hatua kali kwa wazazi na walezi Wilayani Tarime Mkoani Mara ambao wanakubali kukeketa watoto wa kike ambao ukimbia ukeketaji kipindi hicho na baada ya zoezi kumalizika mabinti hao waliokimbia ukamatwa na kukeketwa hivyo wameiomba serikali kuendelea kusimamia vikali sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 ili kutokomeza suala la ukeketaji kwa mtoto wa kike huku baadhi yao wakikeketwa usiku.

Hayo yamebainisha na baadhi ya wazazi katika kata ya Pemba kipindi wakipatiwa elimu ya kupinga Ukeketaji kupitia Shirika la Tanzania Mindset Network chini ya Ufadhili wa TGNP Mtandao kupitia Shirika la Idadi ya Watu Ulimwenguni UNFPA.

Wazazi hao wamedai kuwa kipindi cha ukeketaji watoto wamekuwakikimbia ili wasikeketwa mpaka msimu wa ukeketaji unamalizika lakini pale wanarudi kijijijini ukamatwa na jamii na kukeketwa kwa Nguvu hivyo wameomba serikali kuwachukulia hatua kali wazazi na walezi watakaoshiriki katika kitendo hicho.

“Pia wazazi hao wamesema kuwa kuna tetesi za watoto wa kike kukeketwa nyakati za usiku baada ya serikali kwa kushirikiana na mashiriki kupinga vikali ukeketaji.Kuna Ngariba tunamfaamu yuko maeneo ya mbali ameibuka hivi karibuni tunajua atakeketa watoto wetu usiku hivyo sasa serikali itambue suala hilo” alisema Mmoja wa wazazi katika kijiji cha Nyabisaga kata ya Pemba.

Eliafile Ndossi ambaye ni mwezeshaji kutoka Shirika la Tanzania Mindset Network akitoa elimu juu ya madhara ya kupinga Ukeketaji kwa viongozi wa Vitongoji, Vijiji pamoja na wazazi na walezi katika kijiji Cha Pemba na Kyoruba.
Ghati Samweli ambaye ni mwezeshaji kutoka Shirikala Tanzania Mindset Network akitoa elimu ya kupinga Ukeketaji baada ya kutembelea moja ya familia katika kijiji cha Nyabisaga Wilayani Tarime Mkoani Mara ambapo watoa elimu hiyo wameamua kufika Nyumba kwa Nyumba lego ni kunusuru mtoto wa kike hasiweze kukeketwa.
Picha ya Pamoja baada ya kutolewa kwa elimu ya kupinga Ukekeytaji katika kijiji cha Nyabisaga.
Eliafile Ndossi ambaye ni mwezeshaji kutoka Shirika la Tanzania Mindset Network akitoa elimu juu ya madhara ya kupinga Ukeketaji kwa viongozi wa Vitongoji, Vijiji pamoja na wazazi na walezi katika kijiji Cha Pemba na Kyoruba.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...