SHIRIKA la Great Hope Foundation leo limetoa tuzo kwa washiriki wa mradi wa UWEZO AWARD katika sherehe zilizofanyika chuo kikuu cha Dar es Salaam leo katika shule za Sekondari za hapa nchini.

 Mradi huu unaendeshwa kwa njia ya mashindano ambapo wanafunzi hushindana kutumia uwezo wao kufanya kazi mbalimbali za kijamii ambazo wao wanachagua kufanya.

UWEZO AWARD ina malengo makuu matano ambayo ni  Kuwatengenezea wanafunzi jukwaa la kujitambua/kufahamu uwezo/vipaji walivyonavyo ( hata vile ambavyo havionekani zaidi darasani.

Kuwapa wanafunzi jukwaa la  kujifunza uongozi  Kuwapa wanafunzi jukwaa la kujifunza kuwajibika na kuwa mstari wa mbele kutatua changamoto zinazoikabili jamii inayowazunguka, Kutambua na kutoa tuzo kwa miradi bunifu iliyofanywa na wanafunzi katika UWEZO AWARD na  Kukuza na kuwajengea wanafunzi ujuzi katika maeneo ambayo wanafunzi wameonesha UWEZO.
Washindi wa kwanza wa tuzo za UWEZO AWARD wakipokea tuzo yao kutoka kwa mgeni rasmi Maida waziri mara baada ya kuibuka kidedea kwa kufanya vizuri zaidi katika mradi huo ulioendeshwa na shirika la Great Hope foundation jijini Dar es Salaam leo. Washiriki hao ambao ni kutoka shule ya sekondari ya Zanaki wamejinyakulia Tofi ya Silva pamoja na safari ya kutembelea mbuga za wanyama hapa nchini.
Washindi wa pili wa tuzo za UWEZO AWARD wakipokea tuzo yao kutoka kwa mgeni rasmi Maida waziri mara baada ya kuibuka kidedea kwa kufanya vizuri zaidi katika mradi huo ulioendeshwa na shirika la Great Hope foundation jijini Dar es Salaam leo.
Washindi wa tatu wa tuzo za UWEZO AWARD wakipokea tuzo yao kutoka kwa mgeni rasmi Maida waziri mara baada ya kuibuka kidedea kwa kufanya vizuri zaidi katika mradi huo ulioendeshwa na shirika la Great Hope foundation jijini Dar es Salaam leo.
  Washindi wa nne wa tuzo za UWEZO AWARD wakipokea tuzo yao kutoka kwa mgeni rasmi Maida waziri mara baada ya kuibuka kidedea kwa kufanya vizuri zaidi katika mradi huo ulioendeshwa na shirika la Great Hope foundation jijini Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya wanafunzi wakionyesha umahili wao katika michezo mbalimbali.
Picha na Avila Kakingo,Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...