Na Mwandishi wetu,
Wanafunzi nchini wametakiwa kujibidisha kusoma vitabu mbalimbali sio kwa malengo ya kufaulu mitihani pekee, bali pia kwa ajili kupata elimu na maarifa mapya yatakayowasaidia kukabiliana na changamoto za maisha.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe Jacqueline Mengi ametoa wito huo jijini Dar es salaam wakati akizindua maktaba ya shule ya Msingi Uzuri, iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa ya Ubungo, ambayo imekarabatiwa na kuwekwa vitabu kwa hisani ya taasisi hiyo.
Mkurugenzi huyo pia amewashawishi wanafunzi wa shule za msingi nchini wa kuanzia darasa la nne hadi la saba kushiriki shindano la Andika Challenge la kuandika na kubuni hadith zenye mafundisho, lililoanzishwa na Taasisi hiyo, na kuwahakikishia kuwa kila mkoa utatoa washindi.
Wakizungumza katika hafla hiyo Afisa Elimu wa Manispaa ya Ubungo Chausiku Masegenya, na Mwenyekiti wa Kamati ya shule Bw. Yassin Shaaban Bakari wameipongeza Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe kwa ufadhili huo unaounga mkono jitihada za serikali za kuboresha utoaji wa elimu nchini.
Aidha Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Sifuni Mbwambo na Mwanafunzi Vivian Herbeth wameipongeza taasisi ya Dr Ntuyabaliwe na kusisitiza kuwa shule hiyo ina maendeleo mazuri kitaalum ingawa inakabiliwa na changamoto mbalimbali, zikiwemo upungufu wa samani hasa kwa walimu, uchakavu wa majengo, na ukosefu wa uzio.
Mgeni
rasmi Afisa Elimu wa Manispaa ya Ubungo Chausiku Masegenya akizungumza
wakati wa hafla fupi ya kuzindua maktaba iliyokarabatiwa na kuwekwa
vitabu kwa hisani ya taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe katika shule hiyo,
iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa ya Ubungo jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe Jacqueline Mengi (kushoto) akizungumza na
wanafunzi pamoja na walimu wa shule ya Msingi Uzuri (hawapo pichani)
wakati wa hafla fupi ya kuzindua maktaba iliyokarabatiwa na kuwekwa
vitabu kwa hisani ya taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe katika shule hiyo,
iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa ya Ubungo jana jijini Dar es Salaam.
Katikati ni Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Uzuri, Bw. Sifuni Mbwambo na
kulia ni Mratibu wa Elimu kata ya Manzese, Laura Tesha.
Baadhi
ya wawakilishi wa wanafunzi wa shule ya msingi Uzuri wakimsikiliza
Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe Jacqueline Mengi (hayupo
pichani) wakati wa hafla fupi ya kuzindua maktaba iliyokarabatiwa na
kuwekwa vitabu kwa hisani ya taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe katika shule
hiyo, iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa ya Ubungo jana jijini Dar es
Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya shule Bw. Yassin Shaaban Bakari akitoa neno la
shukrani kwa taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe kwa kukarabati jengo la maktaba
pamoja na kuweka vitabu wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa maktaba hiyo
iliyofanyika katika shule hiyo, iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa ya
Ubungo jana jijini Dar es Salaam.
Mwalimu
Mkuu wa shule ya Msingi Uzuri, Bw. Sifuni Mbwambo, Mkurugenzi wa
Taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe Jacqueline Mengi pamoja na Mratibu wa Elimu
kata ya Manzese, Laura Tesha wakitazama picha za maktaba ilivyokuwa hapo
awali kabla ya kufanyiwa ukarabati na taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe wakati
wa hafla ya kuzindua jengo la maktaba hiyo iliyofanyika katika shule
hiyo, iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa ya Ubungo jana jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe Jacqueline Mengi akikata utepe kuzindua
eneo la maktaba iliyokarabatiwa na kuwekwa vitabu kwa hisani ya taasisi
ya Dr. Ntuyabaliwe katika shule hiyo, iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa
ya Ubungo jana jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mwalimu
Mkuu wa shule ya Msingi Uzuri, Bw. Sifuni Mbwambo (kulia), Mwenyekiti
wa Kamati ya shule Bw. Yassin Shaaban Bakari (katikati), Mratibu wa
Elimu kata ya Manzese, Laura Tesha (kushoto) pamoja na baadhi ya
wanafunzi wa shule hiyo wakiwakilisha wenzao.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe Jacqueline Mengi na Mwalimu Mkuu wa shule
ya Msingi Uzuri, Bw. Sifuni Mbwambo wakifunua pazia kwenye kibao maalum
cha wafadhili ambao ni taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe waliohusika
kukarabati na kuweka vitabu kwenye jengo la maktaba hiyo shuleni hapo
wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa maktaba hiyo iliyofanyika katika
shule hiyo, iliyopo Kata ya Manzese, Manispaa ya Ubungo jana jijini Dar
es Salaam. Anayeshuhudia ni Mwenyekiti wa Kamati ya shule Bw. Yassin
Shaaban Bakari (kulia).
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...